Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 9/1 uku. 15
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Maisha ya Yesu ya Kijamaa Hapo Mwanzoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Maisha ya Mapema ya Jamaa ya Yesu
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Je, Umepata Kujiuliza?
    Amkeni!—1996
  • Yesu Alijifunza Kutii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 9/1 uku. 15

Je, Wajua?

Je, Yesu alikuwa na uhusiano wa kiukoo na yeyote kati ya mitume wake 12?

▪ Maandiko hayatoi jibu lililo wazi kuhusu swali hilo. Hata hivyo, kwa kuzingatia habari fulani na kulingana na mapokeo, inaonekana kwamba mitume fulani kati ya wale mitume 12 walikuwa na uhusiano wa kiukoo na Yesu.

Waandikaji wa vitabu vya Injili wanataja majina ya wanawake waliokuwa wakimtazama Yesu akiwa juu ya mti wa mateso kabla ya kufa. Yohana 19:25 inawataja wanne kati yao: “Mama yake [Maria] na dada ya mama yake; Maria mke wa Klopa, na Maria Magdalene.” Unapolinganisha mstari huo na maelezo yanayopatikana katika kitabu cha Mathayo na Marko kuhusu simulizi hilohilo, unaweza kusema kwamba dada ya mama ya Yesu alikuwa Salome. Yaelekea Salome alikuwa mama ya wana wa Zebedayo. (Mathayo 27:55, 56; Marko 15:40) Mahali pengine wana hao wanatajwa kuwa Yakobo na Yohana, hivyo inawezekana walikuwa binamu wa karibu wa Yesu. Yesu aliwaita ndugu hao wawili ambao walikuwa wavuvi, wawe wanafunzi wake.—Mathayo 4:21, 22.

Maelezo mengine ya kimapokeo yanadai kwamba Klopa, au Alfayo, mume wa mmoja wa wanawake wanaotajwa katika andiko la Yohana 19:25, alikuwa ndugu mkubwa wa Yosefu, baba mlezi wa Yesu. Ikiwa mapokeo hayo ni ya kweli, basi Yakobo mwana wa Alfayo, mmoja kati ya wale mitume 12, alikuwa pia binamu ya Yesu.—Mathayo 10:3.

Yesu na Yohana Mbatizaji walikuwa na uhusiano gani wa kiukoo?

▪ Watu fulani wanaamini kwamba watu hao wawili walikuwa binamu wa mbali. Imani hiyo inategemea tafsiri isiyo sahihi katika andiko la Luka 1:36. Kwa mfano, katika mstari huo, Biblia tafsiri Neno Agano Jipya inasema kwamba Elisabeti, mama ya Yohana, alikuwa binamu ya Maria, mama ya Yesu.

Hata hivyo, ukweli ni kwamba neno la Kigiriki cha awali lililotumiwa katika mstari huo halitaji waziwazi uhusiano wao. Linaonyesha tu kwamba wanawake hao wawili walikuwa na uhusiano fulani, lakini haimaanishi walikuwa binamu. Kama vile kitabu The Interpreter’s Dictionary of the Bible kinavyosema, “maana ya neno hilo ni pana sana hivi kwamba haliwezi kutusaidia kuamua walikuwa na uhusiano wa aina gani.” Hata hivyo, wazo la kwamba Yesu na Yohana walikuwa binamu lilitoka wapi? Kitabu cha marejeo, The Catholic Encyclopedia, kinasema: “Habari zote tulizo nazo kuhusu . . . wazazi wa Maria . . . zilitoka katika vitabu vya apokrifa.”

Kwa hiyo, Yesu na Yohana walikuwa na uhusiano wa mbali wa kiukoo hata ingawa si lazima iwe walikuwa binamu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki