Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 12/1 uku. 3
  • Kinachowachochea Watu Washerehekee Krismasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kinachowachochea Watu Washerehekee Krismasi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Ni Lazima Wewe Usherehekee Krismasi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekei Krismasi?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Krismasi Inamaanisha Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Mizizi ya Krismasi ya Kisasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 12/1 uku. 3

Kinachowachochea Watu Washerehekee Krismasi

“Ni rahisi kunaswa na pilikapilika za majira ya Krismasi. Desturi za sikukuu zinafuatwa tu ili kutimiza wajibu, wakati unaotumiwa pamoja na familia na marafiki unaweza kuwa mfupi kwa sababu ya ratiba zenye shughuli nyingi. Wakati fulani tunakosa shangwe tunayopaswa kuwa nayo kwa sababu ya mikazo tunayopitia.”​—BRAD HENRY, GAVANA WA ZAMANI WA OKLAHOMA [MAREKANI], DESEMBA 23, 2008.

MAJIRA ya Krismasi yanapokaribia, nyimbo, sinema, na vipindi vya televisheni huchochea hisia za shangwe na furaha​—mambo yanayowafanya watu washerehekee Krismasi. Unafikiri ni jambo gani hasa linalopaswa kuwachochea watu? Je, huenda ni

  • Kumkumbuka Yesu Kristo?

  • Kushiriki furaha ya kutoa?

  • Kuwasaidia watu wenye uhitaji?

  • Kutumia wakati pamoja na familia?

  • Kudumisha amani?

Kama alivyosema Gavana Henry, aliyenukuliwa upande wa kushoto, wengi wanaosherehekea Krismasi wanaona ni vigumu kutimiza mambo hayo wakati wa sikukuu. Mara nyingi, wakati wa Krismasi huwa wenye shughuli nyingi, mikazo mingi, na zaidi ya yote ni wakati wa biashara. Je, inawezekana kupata shangwe na upendo, sifa zinazopaswa kuwa sehemu ya Krismasi?

Biblia inatutia moyo tumkumbuke Yesu Kristo, tuwe wakarimu katika kutoa, tuwasaidie wenye uhitaji, na tutumie wakati pamoja na familia zetu. Pia, inatufundisha jinsi ya kufanya amani. Kwa hiyo, badala ya kuzungumzia kwa nini watu fulani hawasherehekei Krismasi,a mfululizo huu utachunguza maswali yafuatayo:

  • Kwa nini watu fulani wanahisi kwamba wanapaswa kusheherekea Krismasi?

  • Kwa nini ni vigumu kutimiza mambo wanayotazamia wakati wa Krismasi?

  • Ni kanuni gani za Biblia ambazo zimewasaidia mamilioni ya watu kupata jambo bora kuliko Krismasi?

a Ili kujua sababu za Kimaandiko zinazowafanya watu fulani wasisherehekee Krismasi, ona makala “Wasomaji Wetu Wanauliza​—Kwa Nini Watu Fulani Hawasherehekei Krismasi?”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki