Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 12/1 uku. 4
  • Kumkumbuka Yesu Kristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumkumbuka Yesu Kristo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kinachowachochea Watu Washerehekee Krismasi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekei Krismasi?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Mizizi ya Krismasi ya Kisasa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Je! Ni Lazima Wewe Usherehekee Krismasi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 12/1 uku. 4

Kumkumbuka Yesu Kristo

“Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”​—LUKA 22:19.

Kwa nini watu fulani husherehekea Krismasi?

Kuhusiana na Krismasi, watu fulani wanasema kwamba “imekusudiwa kumkumbuka Yesu.” Wanasherehekea Krismasi ili kukumbuka siku ya kuzaliwa kwake.

Kwa nini ni vigumu kufanya hivyo?

Miziki na desturi nyingi za Krismasi hazihusiani na Yesu Kristo. Mamilioni ya watu wanaosherehekea Krismasi hawamwamini; baadhi yao hata hawaamini kwamba aliwahi kuwapo. Katika ulimwengu wa kibiashara, Krismasi imekuwa sikukuu ya kutangaza biashara badala ya siku ya kumkumbuka Yesu.

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutusaidia?

“Mwana wa binadamu alikuja . . . kutoa nafsi yake iwe fidia badala ya wengi.” (Marko 10:45) Yesu alisema maneno yaliyonukuliwa mwanzoni mwa makala hii, si katika siku yake ya kuzaliwa bali usiku uliotangulia kifo chake. Jioni hiyo, alianzisha sherehe ndogo ya kukumbuka kifo chake. Hata hivyo, kwa nini Yesu alitaka wafuasi wake wakumbuke kifo chake badala ya kuzaliwa kwake? Kwa sababu dhabihu ya fidia ya Yesu inawapa wanadamu watiifu fursa ya kupata uzima wa milele. Biblia inasema: “Mshahara ambao dhambi hulipa ni kifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzima wa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.” (Waroma 6:23) Hivyo, kila mwaka, kwenye ukumbusho wa kifo chake, wafuasi wa Yesu humkumbuka Yesu Kristo, si kama mtoto mchanga bali kama “mwokozi wa ulimwengu.”​—Yohana 4:42.

“Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake kwa ukaribu.” (1 Petro 2:21) Ili kumheshimu na kumkumbuka Yesu, unapaswa kuchunguza mfano alioweka akiwa mwanamume mkamilifu na mwenye akili. Pia, tafakari jinsi Yesu alivyoonyesha huruma, subira, na ujasiri wa kufanya yale yaliyofaa na utafute fursa za kumwiga Yesu katika maisha yako.

“Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.” (Ufunuo 11:15) Unapomkumbuka Yesu Kristo, fikiria kile anachofanya sasa. Yesu anatawala akiwa Mfalme mbinguni. Neno la Mungu lilitabiri hivi kumhusu Yesu: “Atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini, atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia.” (Isaya 11:4) Sifa hizo zote zenye kuvutia si za mtoto mchanga, bali ni za Mtawala mwenye nguvu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki