Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 9/1 uku. 6
  • Kazi Yetu Inagharimiwaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Yetu Inagharimiwaje?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova Hutumiaje Michango?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Kazi Yetu ya Ulimwenguni Pote Inagharimiwaje?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Yote Hayo Hugharimiwaje?
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Jinsi Kazi za Ufalme Zinavyogharimiwa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 9/1 uku. 6
Mtu akiweka mchango wa hiari kwenye kisanduku cha michango

HABARI KUU | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Kazi yetu inagharimiwaje?

Kila mwaka, tunachapisha na kugawanya mamilioni ya Biblia na machapisho yanayotegemea Biblia. Tunajenga na kuendesha viwanda vya uchapishaji na ofisi za tawi ulimwenguni pote. Makutaniko mengi hukutana katika nyumba za ibada zinazoitwa Majumba ya Ufalme. Ni nani hulipia gharama hizo?

Kazi yetu hutegemezwa kwa michango ya hiari. (2 Wakorintho 9:7) Katika mwaka wa 1879, toleo la pili la gazeti hili lilisema hivi: “Tunaamini kwamba gazeti ‘Zion’s Watch Tower’ [kama lilivyokuwa likiitwa gazeti hili wakati huo] linategemezwa na YEHOVA, na maadamu hivyo ndivyo ilivyo halitawaomba watu wala kuwasihi kamwe walitegemeze.” Bado tunaendelea na sera hiyo.

Michango hutumwa moja kwa moja katika mojawapo ya ofisi zetu za tawi au huwekwa katika sanduku la michango linalopatikana katika kila Jumba la Ufalme. Hata hivyo, hatutoi sehemu ya kumi, hatuchukui sadaka, au kulipisha watu kwa ajili ya huduma zetu au machapisho yetu. Hatulipwi pesa kwa sababu ya kazi ya kuhubiri, kufundisha katika kutaniko, au kusaidia kujenga majengo ya ibada. Yesu alisema hivi: “Mlipokea bure, toeni bure.” (Mathayo 10:8) Watumishi wote wanaofanya kazi katika ofisi za tawi na katika makao makuu, kutia ndani Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, ni washiriki wa kikundi cha kidini wasiolipwa mshahara.

“Kama ilivyo katika utendaji wowote wa Mashahidi wa Yehova, shughuli za dini yao huendeshwa kwa michango ya hiari na kila mtu anaamua kiasi na kadiri atakavyotoa ‘michango’ yake.’”​—Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu, 2011

Michango hutumiwa pia kusaidia wakati wa majanga ya asili. Wakristo wa mapema walifurahia kuwasaidia ndugu zao waliopatwa na matatizo. (Waroma 15:26) Sisi pia huwasaidia wale waliopatwa na maafa kwa kujenga tena nyumba zao na nyumba za ibada, kwa kuwapatia chakula, mavazi, na matibabu.

Kijana mdogo akitabasamu

Tazama video Kimbunga Nchini Filipino—Imani Iliwawezesha Kushinda Matatizo kwenye www.jw.org/sw. (Tafuta kwenye KUTUHUSU > UTENDAJI)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki