BIBLIA INASEMA NINI?
Ni nini hutupata tunapokufa?
BAADHI YA WATU WANAAMINI kwamba tunaendelea kuwa hai tukiwa na mwili wa aina nyingine, na wengi wanahisi kwamba kifo ni mwisho wa kila kitu. Unaamini nini?
BIBLIA INASEMA HIVI:
“Wafu, hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5) Uhai hukoma tunapokufa.
MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA
Adamu, mwanaume wa kwanza, alirudi katika mavumbi alipokufa. (Mwanzo 2:7; 3:19) Vivyo hivyo, watu wote hurudi mavumbini wanapokufa.—Mhubiri 3:19, 20.
Mtu anapokufa, anaondolewa au husamehewa dhambi zake. (Waroma 6:7) Mtu akifa hapewi adhabu yoyote nyingine ili kulipia dhambi zake.
Je, wafu wataishi tena?
UNGEJIBUJE SWALI HILO?
Ndiyo
Hapana
Labda
BIBLIA INASEMA HIVI:
“Kutakuwa na ufufuo.” —Matendo 24:15.
NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?
Mara nyingi Biblia inafananisha kifo na usingizi. (Yohana 11:11-14) Mungu anaweza kumwamsha mtu aliyekufa kama vile tunavyoweza kumwamsha mtu aliyelala.—Ayubu 14:13-15.
Biblia ina masimulizi kadhaa ya ufufuo yanayotupatia uhakika wa kuamini kwamba wafu watafufuliwa.—1 Wafalme 17:17-24; Luka 7:11-17; Yohana 11:39-44.