Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w18 Mei uku. 32
  • Mavuno Tele!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mavuno Tele!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Timiza Huduma Yako Kikamili
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Kueneza Eneo Lililo Peke Yalo Katika Paraguai Kwazaa Tunda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
w18 Mei uku. 32
Kusanyiko la wilaya katika mji wa Nyzhnya Apsha, Ukrainia, mwaka wa 2012

Kusanyiko la wilaya katika mji wa Nyzhnya Apsha, Ukrainia, mwaka wa 2012

Mavuno Tele!

YESU alitabiri kwamba wafuasi wake wangefurahia mavuno tele katika kipindi hiki cha siku za mwisho. (Mt. 9:37; 24:14) Fikiria jinsi maneno yake yalivyothibitika kuwa kweli katika njia ya pekee kwenye eneo la Transcarpathia, Ukrainia. Katika miji mitatu tu iliyo karibu-karibu kwenye eneo hilo, kuna makutaniko 50, na zaidi ya wahubiri 5,400.a Kihalisi, idadi ya watu wote wa miji hiyo inapojumlishwa, mtu mmoja kati ya wanne ni Shahidi wa Yehova!

Itikio la watu katika maeneo hayo likoje? Ndugu mwenyeji anayeitwa Vasile, anasema hivi: “Watu wa hapa wanaheshimu Biblia, wanazingatia haki, wana uhusiano wa karibu wa kifamilia, na hujitahidi kutoka moyoni kusaidiana.” Anaongeza hivi: “Si nyakati zote ambazo wao hukubaliana na mambo tunayoamini. Lakini unapowaonyesha jambo fulani kutoka katika Biblia, wao husikiliza kwa makini.”

Bila shaka, ndugu zetu hukabili changamoto za kipekee wanapohubiri katika eneo ambalo wahubiri ni wengi ikilinganishwa na idadi ya watu wanaopaswa kuhubiriwa. Kwa mfano, kutaniko fulani lina wahubiri 134 lakini eneo wanalopaswa kuhubiri lina nyumba 50 tu! Wahubiri wanakabilianaje na hali hiyo?

Ndugu na dada wengi hujitolea kuhubiri katika maeneo ambako kuna uhitaji mkubwa wa wahubiri. Ionash, ndugu mwenye umri wa miaka 90 anasema hivi: “Uwiano wa wahubiri kwa nyumba zilizo katika eneo la kutaniko letu ni 1 kwa 2. Kwa sasa ninahubiri hapa katika eneo la nyumbani baada ya afya yangu kuzorota, lakini kabla ya hapo nilikuwa nikisafiri kilomita 160 kwenda katika eneo ambalo halijagawiwa kutaniko lolote ambako nilihubiri kwa Kihungaria.” Ni lazima wahubiri wajidhabihu ili kusaidia katika maeneo mengine. Ionash anaendelea kusema hivi: “Ili niwahi kupanda gari-moshi nilihitaji kuamka saa 10 alfajiri na kuhubiri hadi saa 12 jioni wakati ambapo gari-moshi lilisafiri kurudi katika mji wa nyumbani. Nilifanya hivyo mara mbili au tatu kwa juma.” Je, alihisi kwamba jitihada zake zilizaa matunda? Anasema hivi: “Nilifurahia sana aina hiyo ya utumishi. Nilipata shangwe ya kusaidia familia fulani iliyoishi eneo la mbali kujifunza kweli.”

Inaeleweka kwamba si kila mtu katika makutaniko ya eneo hili anayeweza kusafiri kwenda eneo la mbali. Lakini wote, kutia ndani wahubiri waliozeeka, hujitahidi kuhubiri eneo lao kikamili. Matokeo ni kwamba katika mwaka wa 2017, idadi ya watu waliohudhuria Ukumbusho katika miji hiyo mitatu ilikuwa mara mbili ya idadi ya wahubiri, yaani, nusu ya idadi ya watu wote katika miji hiyo. Bila shaka, haidhuru mahali tunapotumikia, bado kuna “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”—1 Kor. 15:58.

a Majina ya miji hiyo ni Hlybokyy Potik, Serednye Vodyane, na Nyzhnya Apsha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki