Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 2 kur. 8-9
  • Mwenzi wa Ndoa Anapofanya Uzinzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwenzi wa Ndoa Anapofanya Uzinzi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAANDIKO YANAYOWEZA KUKUSAIDIA
  • Kushinda Vipingamizi kwa Kuweka Miradi
    Amkeni!—2001
  • Faraja Wakati wa Matatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Je, Kupatana Kwawezekana?
    Amkeni!—1999
  • Nilichagua kazi inayofaa
    Amkeni!—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 2 kur. 8-9
Mwanamke akisali

Mwenzi wa Ndoa Anapofanya Uzinzi

“Nilitamani kufa mume wangu aliponiambia ananiacha ili amwoe mwanamke mwingine mwenye umri mdogo. Niliona amenitendea isivyo haki kabisa, hasa nilipokumbuka jinsi nilivyojidhabihu kwa ajili yake.”​—Maria, Hispania.

“Mke wangu aliponiacha ghafla, nilihisi kana kwamba sehemu fulani ya mwili wangu imekufa. Ndoto zetu, matarajio yetu, mipango yetu; vyote vilitokomea. Kuna nyakati nilihisi jambo hilo halinihangaishi, lakini hali ya kusononeka ilijirudia tena na tena.”​—Bill, Hispania.

INAUMIZA sana mwenzi wa ndoa anapofanya uzinzi. Baada ya kuombwa msamaha, wenzi fulani wameamua kuwasamehe wenzi wao waliowasaliti, na kujenga upya uhusiano wao.a Lakini iwe ndoa hiyo itasitawi tena au la, wenzi wanaogundua kwamba mwenzao ametoka nje ya ndoa, huhisi maumivu makali sana. Hivyo basi, mtu aliyesalitiwa anaweza kukabilianaje na maumivu hayo?

MAANDIKO YANAYOWEZA KUKUSAIDIA

Wenzi wengi ambao wamesalitiwa, wamehisi vizuri baada ya kuchunguza Maandiko, licha ya maumivu makali wanayohisi. Wamejifunza kwamba Mungu anaona kilio chao na anahisi uchungu walio nao.​—Malaki 2:13-16.

“Mahangaiko yaliponilemea, ulinifariji na kunibembeleza.”​—Zaburi 94:19.

Bill anasema: “Niliposoma andiko hilo, nilimwazia Yehova akinibembeleza kwa wororo, kama ambavyo baba mwenye huruma angefanya.”

“Kwa mtu mshikamanifu unatenda kwa ushikamanifu.”​—Zaburi 18:25.

Carmen, ambaye mume wake alikuwa akitoka nje ya ndoa yao kwa miezi kadhaa, anasema: “Mume wangu alinisaliti. Lakini niliamini kwamba Yehova angebaki mshikamanifu kwangu. Hangenivunja moyo.”

“Msihangaike kuhusiana na jambo lolote, bali katika kila jambo kwa sala na dua . . . mjulisheni Mungu maombi yenu; na amani ya Mungu inayozidi uelewaji wote itailinda mioyo yenu.”​—Wafilipi 4:6, 7.

Sasha anasema: “Nilisoma andiko hilo tena na tena. Kadiri nilivyosali, Mungu alinisaidia kupata amani.”

Kuna nyakati ambazo watu wote hao walionukuliwa, walihisi wanaelekea kukata tamaa. Lakini walimtegemea Yehova Mungu na walipata nguvu kupitia Neno lake. Bill alisema hivi: “Imani yangu iliniwezesha kuwa na kusudi la kuishi wakati ambapo nilihisi maisha yangu yamevurugika. Licha ya kwamba kwa kipindi fulani nilitembea ‘katika bonde lenye kivuli kizito,’ Mungu alikuwa pamoja nami.”—Zaburi 23:4.

a Ili kujua mengi zaidi kuhusu uamuzi wa kusamehe au kutomsamehe mwenzi aliyekusaliti, soma mfululizo wenye kichwa “Mwenzi Anapokosa Uaminifu,” kwenye gazeti Amkeni! la Aprili 22, 1999.

Mambo Ambayo Yamewasaidia Wengine

Kutafakari kuhusu Maandiko yanayofariji.

Bill anasema: “Nilisoma kitabu cha Ayubu kisha nikasoma Zaburi, na nilipigia mstari kila kifungu ambacho kiliendana na hali yangu. Niligundua kwamba watu niliosoma kuwahusu walikabili hali zilizowasababishia uchungu na mahangaiko moyoni kama mimi.”

Kusikiliza na kucheza muziki ili kupata faraja.

Carmen anasema: “Usiku niliposhindwa kulala, nilisikiliza muziki. Nilifarijika sana.” Daniel anaelezea: “Nilijifunza kucheza gitaa, na muziki niliocheza ulinisaidia kuhisi amani moyoni na utulivu.”

Kufunua hisia zao.

Daniel anasema: “Mwanzoni, sikuwa na kawaida ya kuwaeleza watu hisia zangu. Lakini nilikuwa na marafiki wazuri, na nilizungumza nao kila siku. Niliwamiminia moyo wangu katika maandishi na kupitia mazungumzo, na hivyo nikatua mzigo niliokuwa nao. Kufanya hivyo kulinisaidia sana.” Sasha anasema: “Familia yangu ilinisaidia sana. Mama yangu alikuwa tayari kunisaidia wakati wowote ule. Nilipohitaji mtu wa kuzungumza naye, alikuwa tayari kunisikiliza. Baba alifanya nihisi bado ninapendwa na niko salama, na alinisaidia nirudie hali yangu ya kawaida bila kunishurutisha.”

Kusali bila kuacha.

Carmen anasema: “Nilisali tena na tena. Nilihisi kwamba Mungu alikuwa karibu nami, akinisikiliza na kunisaidia. Katika kipindi hicho kigumu, nilimkaribia Mungu zaidi.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki