Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 2 kur. 12-13
  • Unapohisi Umelemewa na Unatamani Kufa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unapohisi Umelemewa na Unatamani Kufa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUNAWEZA KUPATA WAPI MSAADA?
  • SULUHISHO LA KUDUMU
  • Kwa Nini Sisi Sote Twapaswa Kumsifu Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Mtu Anahisije Anaposhuka Moyo?
    Amkeni!—2009
  • Kulishinda Pigano Dhidi ya Mshuko wa Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Msaada Kutoka kwa “Mungu wa Faraja”
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 2 kur. 12-13
Mwanamke ameketi akiwa na Biblia iliyo wazi akitazama mbali

Unapohisi Umelemewa na Unatamani Kufa

Adriana, anayeishi Brazili, anasema: “Hisia hizo ziliniandama sana. Hivyo, niliona ni afadhali tu nijiue.”

JE, UMEWAHI kuhisi vibaya sana mpaka ukatamani kufa? Ikiwa ndivyo, basi unaweza kuelewa hali ya Adriana. Alikuwa na wasiwasi na mawazo tele na alihuzunika sana na kujihisi hana tumaini. Adriana alikuwa na ugonjwa wa kushuka moyo.

Fikiria pia kisa cha Kaoru, mwanamume anayeishi Japani aliyekuwa akiwauguza wazazi wake waliozeeka. Anasema: “Wakati huo, nilihisi nimelemewa sana kwa sababu ya mkazo niliopata kazini. Baada ya muda nilipoteza hamu ya kula, na nikaanza kukosa usingizi. Nilianza kuhisi kuwa nikifa nitakuwa nimetua mzigo.”

Ojebode, anayeishi Nigeria, anasema hivi: “Nilikuwa mwenye huzuni nyakati zote jambo lililofanya nilie, na hivyo nilitafuta njia ya kujiua.” Jambo lenye kupendeza ni kwamba Ojebode, Kaoru, na Adriana hawakujiua. Hata hivyo, kila mwaka, mamia ya maelfu ya watu hujiua.

TUNAWEZA KUPATA WAPI MSAADA?

Idadi kubwa ya watu wanaojiua ni wanaume, na wengi wao hufikia hatua hiyo kwa sababu wanaona aibu kuomba msaada. Yesu alisema kwamba wagonjwa wanahitaji daktari. (Luka 5:31) Hivyo, ikiwa unapata mawazo ya kujiua, tafadhali usisite kutafuta msaada. Watu wengi wenye ugonjwa wa kushuka moyo wamegundua kwamba kupata matibabu huwasaidia kukabiliana na hali yao. Ojebode, Kaoru, na Adriana walipata matibabu na sasa wanaendelea vizuri.

Madaktari wanaweza kumtibu mgonjwa aliye na tatizo la kushuka moyo kwa kutumia dawa au kwa kuzungumza naye ili arekebishe hisia na mawazo yake, au huenda wakatumia mbinu zote mbili. Kwa kuongezea, watu walioshuka moyo wanahitaji familia na marafiki wao wawaelewe na kuwatunza kwa upendo na subira. Yehova Mungu ndiye rafiki bora, na kupitia Neno lake Biblia, yeye hutoa ushauri na faraja.

SULUHISHO LA KUDUMU

Mara nyingi, wale walio na tatizo la kushuka moyo wanahitaji matibabu ya kuendelea, na inabidi wabadilishe njia yao ya maisha. Lakini ikiwa una tatizo hilo utafurahi kujua kwamba hali itakuwa nzuri wakati ujao. Ojebode ana tumaini hilo, na anasema: “Ninatazamia kuona andiko la Isaya 33:24 likitimia. Linatabiri kwamba wakati ujao hakuna yeyote duniani atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’” Kama Ojebode, unaweza kupata faraja kwa kufikiria ahadi ya Mungu ya “dunia mpya.” Ahadi hiyo itakapotimia, “maumivu” hayatakuwepo tena. (Ufunuo 21:1, 4) Matatizo yote ya akili na ya kihisia yataondolewa. Hisia zote mbaya ulizonazo hazitakuwepo tena. Mambo yanayokuumiza “hayataingia tena akilini, wala hayataingia tena moyoni [mwako].”—Isaya 65:17.

Maandiko Yanayoweza Kukusaidia

Mungu anaelewa hisia zako.

“Mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika kwa nguvu mkono wako wa kulia, . . . [ninakwambia], ‘Usiogope. Nitakusaidia.’”​—Isaya 41:13.

Yehova anaelewa hisia zetu vizuri sana kuliko mtu mwingine yeyote, na anataka kutusaidia.

Tafakari ujumbe wa Neno la Mungu.

“[Eliya] akaomba afe. Akasema: ‘ . . .  Ee Yehova, niue.’”​—1 Wafalme 19:4.

Ojebode anasema: “Kutafakari ujumbe wa Neno la Mungu kulinisaidia. Nilitambua kwamba nabii Eliya alihisi kama mimi nilivyohisi.”

Jifunze kutokana na masimulizi ya Biblia.

“Nimeomba dua kwa ajili yako [Petro] ili imani yako isidhoofike.”​—Luka 22:32.

Baada ya kumkana Yesu mara tatu, mtume Petro alilemewa sana na hisia hivi kwamba akalia kwa uchungu. Kaoru anasema: “Simulizi la Petro lilinisaidia kutambua kwamba Yehova na Yesu walijali hisia za Petro. Hilo lilinitia moyo sana.”

Mambo yanayokuumiza “hayataingia tena akilini, wala hayataingia tena moyoni [mwako].”​—Isaya 65:17

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki