Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 3 kur. 14-15
  • Inawezekana Kufurahia Maisha Hata Sasa​—Jinsi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Inawezekana Kufurahia Maisha Hata Sasa​—Jinsi Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KURIDHIKA NA MAISHA YETU
  • KUKABILIANA NA MATATIZO YA AFYA
  • KUIMARISHA NDOA
  • Funguo Mbili za Kuwa na Ndoa Yenye Kudumu
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Maisha ya Jamaa—Namna Unavyoweza Kufanikiwa
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Kujenga Maisha ya Furaha ya Jamaa
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Tabasamu Ni Yenye Manufaa Kwako!
    Amkeni!—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 3 kur. 14-15
Mwanasayansi mmoja aliyetajwa mwanzoni akipika chakula pamoja na mke wake
Mwanasayansi mmoja aliyetajwa mwanzoni akipika chakula pamoja na mke wake

Inawezekana Kufurahia Maisha Hata Sasa—jinsi Gani?

KUISHI bila kuugua, kuzeeka, na kufa—hayo ni maisha ambayo wewe pia, unaweza kufurahia wakati ujao! Hata hivyo, leo maisha yamejaa changamoto na matatizo chungu nzima. Unaweza kuboreshaje hali zako sasa? Biblia ina ushauri unaoweza kukusaidia kuwa na maisha yenye furaha na yanayoridhisha hata sasa. Hebu tuchunguze baadhi ya matatizo na jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia.

KURIDHIKA NA MAISHA YETU

Ushauri wa Biblia: “Njia yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa, huku mkiridhika na vitu mlivyo navyo.”—Waebrania 13:5.

Kila siku, bidhaa na huduma zinazosemekana kuwa za lazima zinazalishwa kwa wingi. Hata hivyo, Biblia inasema inawezekana ‘kuridhika na vitu tulivyo navyo.’ Jinsi gani?

Kwa kuepuka “kupenda pesa.” Watu wako tayari kufanya chochote hata kama kitaathiri afya yao, familia, na urafiki, au kushusha maadili na heshima waliyo nayo—yote kwa sababu ya “kupenda pesa.” (1 Timotheo 6:10) Wanachopoteza hakiwezi kulinganishwa hata kidogo na wanachotafuta! Na kwa vyovyote vile, mtu anayependa mali “hatatosheka.”—Mhubiri 5:10.

Kuwathamini watu, na si vitu. Ni kweli kwamba vitu vya kimwili ni muhimu. Lakini vitu haviwezi kuonyesha kwamba vinatupenda au kututhamini; wanadamu wenzetu tu ndio wenye uwezo huo. Kuwa na “rafiki wa kweli” hutusaidia kuridhika na maisha.—Methali 17:17.

TUNAWEZA KUFURAHIA MAISHA HATA SASA IKIWA TUTAFUATA MWONGOZO WA BIBLIA

KUKABILIANA NA MATATIZO YA AFYA

Ushauri wa Biblia: “Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri.”—Methali 17:22.

Kama “dawa nzuri,” kuwa na shangwe kunaweza kukusaidia kupambana na matatizo ya afya. Lakini unawezaje kuwa mwenye shangwe ilhali afya yako si nzuri?

Uwe mwenye shukrani. Tukikazia fikira matatizo yetu tu, “kila siku” itaonekana kuwa mbaya. (Methali 15:15, Biblia Habari Njema) Badala yake, Biblia inasema, ‘uwe mwenye shukrani.’ (Wakolosai 3:15) Jitahidi kuthamini mambo mazuri maishani, hata yawe madogo, kama kuangalia jua likitua, kupulizwa na upepo mwanana, au kumwona mtu unayempenda akitabasamu. Mambo haya hufanya tufurahie maisha.

Wasaidie wengine. Hata ikiwa tuna matatizo ya afya, “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Wengine wanapoonyesha wanathamini jitihada zetu, hisia nzuri hufurika kwenye moyo wetu, na hivyo kufanya tusahau matatizo tuliyo nayo. Tunaweza kufurahia maisha yetu kwa kuwasaidia wengine kupata furaha.

KUIMARISHA NDOA

Ushauri wa Biblia: “Mhakikishe mambo muhimu zaidi.”—Wafilipi 1:10.

Wenzi wanapotumia muda mchache pamoja, ukaribu wao unaweza kuanza kufifia. Kwa hiyo, ni jambo la busara kwa mume na mke kuitanguliza ndoa yao, kwa kuwa ndoa ni kati ya mambo muhimu zaidi maishani.

Fanyeni mambo pamoja. Badala ya kufanya mambo yanayokupendeza kibinafsi, kwa nini msipange mambo hususa ambayo mtafanya pamoja? Biblia inasema: “Wawili ni afadhali kuliko mmoja.” (Mhubiri 4:9) Mnaweza kupika pamoja, kufanya mazoezi, kwenda kutembea pamoja, kufurahia mlo na vinywaji pamoja, au kutazama mpira pamoja.

Mwonyeshe mwenzi wako kwamba unampenda. Biblia inawahimiza waume na wake wawe na heshima na wapendane. (Waefeso 5:28, 33) Kutabasamu kwa uchangamfu, kumkumbatia mwenzi wako kwa upendo, au kumpatia zawadi ndogondogo ni mambo yanayoweza kuimarisha sana ndoa yenu. Ni muhimu kuzingatia kwamba, wenzi hawapaswi kuonyesha upendo wa kimahaba kwa mtu mwingine tofauti na mwenzi wao.—Waebrania 13:4.

“HATIMAYE, NIMEPATA KUSUDI MAISHANI!”

—Simulizi la Ryoko Miyamoto, Japani.

Maisha yalikuwa magumu. Mume wangu alikuwa mlevi sana na hakuweza kudumisha kazi. Alikataa kuwatunza watoto wetu wanne. Licha ya kufanya kazi kwa bidii, niliona giza tu mbele yangu. Nilikuwa nikijiuliza, ‘Je, hivi ndivyo maisha yangu yalivyopangwa kuwa, ama hii ni adhabu ya makosa niliyofanya awali?’

Kisha, nikatembelewa na Shahidi wa Yehova. Akiwa ametabasamu, alizungumza kwa uchangamfu kuhusu Ufalme wa Mungu na uzima wa milele. Alianza kunifundisha Biblia. Nilijifunza kwamba Mungu yupo, na ana hekima, hutenda kwa haki, na ni mwenye upendo. Pia, nilijifunza kuhusu hali ya wafu, na kwamba mateso niliyokuwa nikipata hayakuwa yamepangwa mapema.

Zaidi ya yote, nilifurahi kujua kwamba njia pekee ya kuwa na maisha yanayoridhisha ni kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Kujua kweli za Biblia kumenifariji, kumeniweka huru, na kunipa utulivu. Hatimaye, nimepata kusudi maishani!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki