Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/89 kur. 1-4
  • Je! Wewe Unatoa Sababu ya Tumaini Lililo Ndani Yako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Unatoa Sababu ya Tumaini Lililo Ndani Yako?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUFIKIA MIOYO YA WASIKILIZAJI
  • KWENYE ZIARA ZA KURUDIA
  • Kaa Chonjo Kutoa Fasihi za Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Vichapo vya Zamani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Mtumaini Yehova na Uwe Hodari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Furahia Tumaini Lisilokatisha Tamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 1/89 kur. 1-4

Je! Wewe Unatoa Sababu ya Tumaini Lililo Ndani Yako?

1 Hivi karibuni ndugu mmoja aliulizwa hivi, “Je! wewe waitikadi kwamba una ile dini pekee ya kweli?” Yeye alijibu hivi: “Bila shaka naitikadi hivyo. Ikiwa sikufikiri hivyo, mimi ningejiunga na nyingine.” Ndipo yeye akaendelea kueleza kwa fadhili zilizo itikadi za Mashahidi wa Yehova na msingi wazo wa Kimaandiko. Yeye alikuwa akifuata onyo la upole “kujibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.”—1 Pet. 3:15.

2 Kila siku, kuna fursa za kutoa sababu ya tumaini letu. Kazini, wafanya kazi wenzi huenda wakataka kujua kwa nini wewe hujitii katika mazungumzo yao yenye kushusha tabia. Shuleni, walimu au wanafunzi wenzi huenda wakauliza kwa nini wewe husherehekei sikukuu. Jirani huenda wakauliza kwa nini wewe huenda mikutanoni mara nyingi sana. Pindi hizo huenda zikaandaa mifungulio ya kutumia shauri la mtume Petro. Ikiwa wewe umekwisha jitayarisha kujibu, huenda wewe ukasaidia waulizaji wenye mioyo myeupe wajifunze kutumikia Yehova pamoja na sisi.

KUFIKIA MIOYO YA WASIKILIZAJI

3 Ili kuwa na mazungumzo na watu, inahitajiwa kabisa kuwa na mambo ambayo mnakubaliana. Hiyo ni kweli tuwe tuko katika utumishi wa shambani au tunazungumza vivi hivi. Kielelezo bora cha Kibiblia kimerekodiwa kwenye Matendo 17:22-31. Angalia jinsi ambavyo kwa ustadi mwingi mtume Paulo aliweka mwanzoni mambo waliyokubaliana na jinsi yeye alivyoyadumisha muda wote wa mazungumzo. Kama tokeo, baadhi yao walisadikishwa juu ya ukweli.—Ona Kiongozi cha Shule, kurasa 156-8, mafungu 15-24.

4 Uendapo mlango kwa mlango katika mwezi wa Januari, tafuta mambo mnayokubaliana ya kuanzishia mazungumzo. Sisi tunaelekeana na matatizo yale yale waliyo nayo wenye nyumba. Hayo yanatia ndani hangaikio la usalama wa watoto wetu na wakati ujao wao, ukosefu wa amani halisi, uhalifu unaoongezeka, na matumizi mabaya ya dawa za kulevya. Ufalme wa Mungu ndio jawabu, kwa hiyo Kichwa cha Mazungumzo chetu kinakazia baadhi ya baraka za Ufalme huo.

5 Makundi ambayo yana vitabu vya kurasa 192 vilivyokusudiwa vitumiwe katika kampeni hii yatavitoa kwa nusu ya mchango wa kawaida. Unapotoa vichapo hivyo, kazia habari hususa inayolenga Ufalme wa Mungu. Mathalani, huenda wewe ukataka kuonyesha kitabu World Government. Katika kurasa 9 hadi 13, kinaelezea ulimwengu ulioonyeshwa katika njozi kwenye Ufunuo 21:4. Life Does Have a Purpose huzungumzia habari inayofanana sana na hiyo kwenye ukurasa 31. Ikiwa vichapo vya zamani havipatikani, kichapo kingine chochote cha kurasa 192 chaweza kutolewa kwa mchango wa kawaida.

KWENYE ZIARA ZA KURUDIA

6 Unaporudi kusitawisha kupendezwa kulikoonyeshwa, jitayarishe kueleza kirefu zaidi sababu ya tumaini lako. Jenga juu ya yale mambo mliyotangulia kukubaliana na mwenye nyumba. Sikiliza rai zake. Sababu pamoja naye. Mwache na tazamio la kwamba ziara za wakati ujao zitaandaa habari zaidi yenye kujenga ambayo juu yayo tunaweza pia kujenga tumaini.

7 Wakati wowote njia inapofunguliwa ya kutoa sababu ya tumaini lililo ndani yetu, sisi tunataka kuitumia kwa manufaa. Tuwe vijana au wazee, yatupasa tuweze kutoa sababu za imani yetu zilizo timamu, wazi, na zenye kushawishi. Sisi sote na tuonyeshe imani imara kwa kutoa kwa bidii sababu ya tumaini letu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki