Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/89 kur. 1-12
  • Fanya Utumishi wa Wakati Wote Uwe Kazi-Maisha Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fanya Utumishi wa Wakati Wote Uwe Kazi-Maisha Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • NJIA YA MAISHA YENYE KUTHAWABISHA
  • UWE MWENYE MAENDELEO KATIKA HUDUMA YAKO
  • Baraka za Huduma ya Painia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Utumishi wa Painia—Je, Wakufaa Wewe?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Upainia Huimarisha Uhusiano Wetu na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 10/89 kur. 1-12

Fanya Utumishi wa Wakati Wote Uwe Kazi-Maisha Yako

1 Kazi inayohusiana moja kwa moja na kutimiza wakfu wetu na kupata uhai wa milele ni huduma ya Kikristo. (Rum. 10:10; 1 Tim. 4:16) Yesu alipowaalika wengine wawe wafuasi wake, aliwafahamisha waziwazi kwamba hii ilitia ndani kujulisha wazi kotekote Ufalme wa Mungu. (Luka 9:57-62) Ingawa kuitikia kwetu mwaliko huu huenda kusihitaji kubadili kazi yetu ya kuajiriwa, kwa wazi kunahusu kubadili mambo tunayotanguliza mbele. Kazi ya maana sana ni “kujulisha wazi sifa bora” za Yehova, ambayo inatia ndani kufanya wanafunzi. (1 Pet. 2:9, NW; Mt. 24:14; 28:19, 20) Basi, wote ambao wamejitoa kwa Yehova kabisa, hufanya maisha yao yategemee huduma hasa. Wengi ambao hali zao za kibinafsi zinawaruhusu wameweza kufanya huduma ya wakati wote iwe kazi-maisha yao.—2 Kor. 4:1, 7.

NJIA YA MAISHA YENYE KUTHAWABISHA

2 Akitazama nyuma kwenye miaka 54 ya utumishi wa wakati wote, painia mmoja alisukumwa na moyo kuandika hivi: “Shangwe ambazo Yehova ametoa zapita kwa mbali dhiki ambazo zimekuwapo. Kama ningepewa fursa za kuishi tena maisha yangu, kwa nia ningetumia wakati wangu wote kumsifu Mungu mkubwa, Yehova.” Hakuna kazi-maisha ya ulimwengu ambayo ingeweza kuleta uradhi na shangwe yenye kina kirefu ambayo inatokana na mwendo huu. Kufuatia maisha ya utumishi wa wakati wote ni wonyesho wa ujitoaji kimungu ambao unatoa sasa thawabu zisizoweza kupimwa na baraka hakika zitakazopatikana wakati ujao.—1 Tim. 4:8.

3 Kazi-maisha katika huduma ya wakati wote inaweza kuleta furaha kubwa sana kwa sababu inahusisha kutoa kwingi sana. (Mdo. 20:35) Urafiki bora sana, ule wa Yehova na Mwana wake Yesu Kristo, unakuzwa na kuimarishwa kwa kujihusisha kikamili zaidi katika masilahi ya Ufalme. (Luka 16:9; 1 Kor. 15:58) Wewe unapata uradhi na dhamiri nzuri kwa kuwa unatenda katika njia ya nafsi nzima kulingana na hali zako. Njia yako ya maisha iliyotiwa nidhamu zaidi inakuwezesha kutimiza mengi kwa kutii amri ya Kristo ya ‘kutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.’—Mt. 6:33, NW.

UWE MWENYE MAENDELEO KATIKA HUDUMA YAKO

4 Kazi-maisha inahusisha kufuatia tendo lenye kuendelea katika uwanja au jitihada fulani. Tendo lenye kuendelea ni la maana ili kuwa na uvumilivu na kudumisha shangwe na bidii ukiwa painia. Kupitia tengenezo lake, Yehova anaandaa elimu ya kiroho kwenye mikutano ya kundi na kwenye makusanyiko. Kuongezea haya ni mikutano pamoja na wazee inayofanywa Desemba na pamoja na mwangalizi wa mzunguko anapozuru. Wakati wa juma la mwangalizi wa mzunguko, kipindi cha pekee kinapangwa kwa ajili ya mapainia. Je! wewe unaandika mambo na kutumia kwa kudhamiria kutumia madokezo mazuri yanayotolewa kwenye mikutano hiyo?

5 Ikiwa wewe huongozi funzo la Biblia lenye maendeleo, je! huu ni mradi wako? Je! unaweza kufanyia maendeleo matangulizi yako kwenye milango au njia unayoshughulika na vipingamizi ambavyo ni vya kawaida katika eneo lenu? Je! umefikiria pendeleo la kufanyia kazi eneo lisilogawiwa mtu au hata kuhama kwa muda au kuhama kabisa ili kusaidia kundi ambalo linahitaji msaada? Katika njia hizi na nyingine nyingi, unaweza kufanya maendeleo katika kazi-maisha yako na kufanya uwezo wako wa kutimiza kazi ya Mungu uwe safi.

6 Ikiwa unafikiria kwa uzito kujiunga na wengi ambao watachukua kazi ya upainia katika miezi inayokuja, dumu katika sala kwa Yehova kuhusu jambo hilo. (Mt. 7:7, 8) Wengi wamejenga tegemeo lao kwa Yehova kwa kutumikia wakiwa mapainia wasaidizi.

7 Si uwezo fulani usio wa kawaida unaomwezesha mtu kufanya upainia. Upendo wa kweli kwa Mungu na kwa watu, pamoja na nia ya kujidhabihu kibinafsi, vinahitajiwa. (Mt. 22:37-39; Flp. 4:13) Huduma ya Kikristo inaweza kukusaidia ukuze sifa ambazo lazima zionekane wazi katika wale ambao wataokoka Har–Magedoni. Kuufuatia wakati wote kunaweza kuongeza upendo, imani, shangwe, na amani yako. (Gal. 5:22, 23) Kwa hiyo jitahidi kufikia na kushikilia huduma ya painia kuwa kazi-maisha yako iliyo hazina!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki