New World Translation Yasaidia Watafutaji Ufalme
1 Isaya alitabiri wakati ambapo “giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabla za watu.” (Isa. 60:2) Wakati huo umefika. Tukiwa “wana wa nuru,” tuna pendeleo la ajabu la kuwapa watu nuru ya kielimu katika eneo letu tulilogawiwa. (Luka 16:8) Wakati wa mwezi wa Novemba, tutafanya hivyo kwa kutoa New World Translation of the Holy Scriptures ili wenye mioyo ya ufuataji haki waweze ‘kutoka gizani wakaingie katika nuru yake ya ajabu.’—1 Pet. 2:9.
2 Biblia inaangaza akili na mioyo ya wale ambao wanaisoma na kuitumia. Hata mamlaka ya kilimwengu imetambua thamani yayo isiyopimika. Mataifa yametegemeza nyingi za sheria zayo za haki kwenye kanuni za uadilifu za Biblia. Inatoa shauri timamu kuhusu jinsi ya kuishi sasa, nayo inaonyesha jambo tunalohitaji kufanya ili tuokoke uharibifu wa ulimwengu unaokuja na kupata uhai wa milele katika ulimwengu mpya wenye uadilifu.—Yoh. 17:3.
THAMANI YA NEW WORLD TRANSLATION
3 New World Translation ni msaada wenye nguvu katika kusaidia watu wa mfano wa kondoo wajifunze ukweli. Kwa kufaa inarudisha jina la Yehova kwenye andiko katika Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki. Inaacha mafungu ya maneno yasiyo halisi, kama yale yanayopatikana kwenye 1 Yohana 5:7. Inafasiri kwa usahihi mafungu ya maneno ambayo yametafsiriwa kimakosa na wengine ambao wamechochewa na mafundisho ya dini bandia, kama vile Utatu. Inatafsiri kwa usahihi lugha za asili katika Kiingereza cha ki-siku-hizi kilicho waziwazi, na chenye kueleweka.
4 Wale ambao wanatafuta Ufalme wa Mungu kwa moyo mweupe watasaidiwa sana kwa kuwa na nakala yao wenyewe ya New World Translation na kuisoma. Tutaitoa pamoja na broshua Jina la Mungu Litakaloendelea Milele. Jitayarishe vizuri kutoa toleo hili. Ratibu wakati ili upitie broshua, ukitafuta mambo ya kuzungumzia ambayo utatumia ukiitoa. Huenda ikawa kwamba broshua itaamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba. Tukifanya ziara ya kurudia kila mahali tulipoangusha broshua, huenda mafunzo ya Biblia yakaanzishwa.
MADOKEZO YENYE MSAADA
5 Matangulizi yaliyo bora sana yanayoweza kutumiwa wakati wa kutoa Biblia yanapatikana kwenye ukurasa 10 wa kitabu Reasoning. Pia, habari inayopatikana kwenye kurasa 58-68 na 276-80 zinaweza kutusaidia tujibu mapingamizi ya wale ambao wana maarifa kidogo kuhusu Neno la Mungu. Habari zaidi juu ya Biblia zinaweza kupatikana kwenye kurasa 307-13 za Insight, Buku 1. Utapata kwamba wakati unaotumia ukitayarisha kwa ajili ya huduma utathibitika kuwa baraka kwako na kwa wale unaonena nao.—1 Tim. 4:13, 15, 16.
6 Kutoa Biblia kunaweza kufanywa katika njia rahisi, ya moja kwa moja. Kwa kielelezo, huenda ukasema: “Utaona kwamba Biblia ninayotumia inatumia lugha iliyo rahisi kuelewa.” Kisha toa sababu kuhusu thamani ya Neno la Mungu na jinsi maarifa yalo yanaweza kuwa yenye manufaa makubwa. Au huenda ukauliza hivi: “Ingawa Biblia ndiyo inayouzwa sana ulimwenguni na makao mengi yana moja, wengi hawaisomi. Tafsiri fulani fulani ni ngumu kuelewa. Kwa hiyo kupata tafsiri ya lugha ya ki-siku-hizi kutakutia moyo usome Neno la Mungu.”
7 Tunaweza kuwa wenye shukrani kama nini kwamba Yehova “ndiye aliyeng’aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu.” (2 Kor. 4:6) Acheni tujitahidi wenyewe katika mwezi wa Novemba ili tufaulu kusaidia wengine waonee shangwe manufaa za New World Translation.