Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/88 kur. 1-8
  • Watie Moyo Wengine Wasome na Kujifunza Neno la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watie Moyo Wengine Wasome na Kujifunza Neno la Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI YA KUTIA MOYO WENGINE
  • KUTOA BIBLIA NA KITABU “UFALME WAKO UJE”
  • New World Translation Yasaidia Watafutaji Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Biblia—Chanzo cha Faraja na Tumaini Katika Ulimwengu Wenye Masumbuko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Kutoa Habari Njema Kutoa Mafunzo ya Biblia Nyumbani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Kutoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 11/88 kur. 1-8

Watie Moyo Wengine Wasome na Kujifunza Neno la Mungu

1 Kati ya vitabu vyote ambavyo vimepata kuandikwa, Biblia peke yake ndiyo inayoandalia aina ya binadamu mwongozo usioshindwa juu ya jinsi ya kushughulika na matatizo ya maisha. (Yer. 10:23) Kuongezea hilo, hiyo inatupa pia tumaini hakika kwa wakati ujao. Ni zawadi ya Mungu kwa mwanadamu. Ingawa Biblia ndiyo bidhaa inayouzwa kwa wingi zaidi sana kwa wakati wote, uchunguzi unaonyesha kwamba asilimia ndogo tu ya wale ambao wana nakala moja ndio wanachukua nafasi ya kuisoma. Je! tunaweza kusaidia watu zaidi wanufaike kutokana na Neno la Mungu lililoandikwa?

2 Hata watu wawe wanaishi wapi duniani, wanakabili matatizo yale yale. Maswali yenye kutatanisha yanahitaji majibu, na ni Biblia peke yayo iliyo na majibu yaliyo sahihi. Kwa nini tupo hapa? Kwa nini watu wanazeeka na kufa? Tunaelekea wapi? Kwa nini kuna ongezeko la uvunjaji wa sheria? Kwa nini Mungu anaruhusu uovu? Kuna suluhisho gani kwa ajili ya infleshoni, ukosefu wa nyumba na upungufu wa chakula, na kadhalika? Tunahitaji kusoma na kujifunza Biblia ili tupate majibu yenye kutosheleza kwa maswali haya na mengine.

JINSI YA KUTIA MOYO WENGINE

3 Ili kutia moyo watu wasome na kujifunza Neno la Mungu, tunahitaji kuingiza ndani yao utumainifu wa kwamba Biblia imevuviwa na Mungu. (2 Tim. 3:16) Tunaweza kufanya hivyo kwa kutumia visehemu vya habari vilivyochaguliwa chini ya kichwa “Biblia” katika kitabu Reasoning. Kurasa 60 hadi 64 zinatoa uthibitisho tofautitofauti kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililovuviwa.

4 Wengi wameanza kusoma Biblia kisha wakaacha. Kwa nini? Labda ni kwa sababu walivunjika moyo kwa kutoelewa wanayosoma. Huenda ikawa kwamba tunaweza kusaidia watu hao kwa kuwatia moyo wasome New World Translation of the Holy Scriptures. Nakala 50,000,000 za tafsiri hii ambayo ni rahisi kusoma na yenye lugha ya ki-siku-hizi zimetolewa katika lugha mbalimbali, hilo likiifanya iwe mojapo tafsiri kuu za Biblia za karne ya 20 zinazotumiwa leo.

5 Wakati wowote tunapopata watu wanaoonyesha upendezi wa kusoma Biblia, tunapaswa kujitoa tujifunze Biblia pamoja nao. Tunapaswa kuonyesha upendezi wa pekee kwa kuwasaidia wale ambao wana New World Translation. Kama ilivyokaziwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba, tunatika kuongoza mafunzo ya Biblia yenye maendeleo. (Mt. 28:19, 20) Hilo linamaanisha kwamba tutajaribu kufikia moyo wa mwanafunzi ili kwamba yale anayojifunza yaweze kuongoza mwenendo wake na kujibu maswali yake ya Biblia.

KUTOA BIBLIA NA KITABU “UFALME WAKO UJE”

6 Wakati wa mwezi wa Novemba, tutaonyesha New World Translation of the Holy Scriptures na kitabu “Ufalme Wako Uje.” Kwa kutoa vichapo viwili hivyo kwa idili, huenda tukaweza kuwatia moyo watu zaidi wasome na kujifunza Neno la Mungu. Huenda ukataka kurekebisha utangulizi ulio chini ya “Uhai/Furaha” kwenye ukurasa 13 wa kitabu Reasoning, uutumie kuwa utangulizi wa Kichwa cha Mazungumzo cha sasa. Au rekebisho la utangulizi wa kwanza chini ya “Jamaa/Watoto” kwenye ukurasa 11 unaweza kukufaa wewe na eneo lako. Kujitayarisha kwa matangulizi hayo mawili kunaweza kukuandaa wewe ili usaidie watu wengi wakati wa Novemba.

7 Tukaribiapo mwisho wa mfumo huu wa mambo, bila shaka watu wengi mmoja mmoja wenye maswali watakuwa wakitafuta majibu ambayo yanaweza kupatikana katika Neno la Mungu peke yake. Na tuwe wenye bidii-endelevu katika kuwatolea wanachohitaji. Na tufulize katika kuwatia moyo wengine wasome na kujifunza Neno la Mungu. Toleo la Novemba la New World Translation na kitabu “Ufalme Wako Uje” linatufungulia njia nzuri ya kufanya hivi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki