Biblia—Chanzo cha Faraja na Tumaini Katika Ulimwengu Wenye Masumbuko
1 Ulimwengu huu huweka wanadamu katika msongo mkali zaidi na katika uhitaji wa faraja na tumaini. Biblia ndiyo chanzo pekee cha faraja ya kweli. Hutoa tumaini la ulimwengu mpya wa uadilifu. (Rum. 15:4; 2 Pet. 3:13) Kitabu Insight, Buku 1, ukurasa 311, chasema hivi: “Bila Biblia hatungemjua Yehova, hatungejua zile manufaa nzuri ajabu zinazotokana na fidia ya dhabihu ya Kristo, na hatungeelewa matakwa yanayohitaji kufikiwa ili kupata uhai wa milele au kuwa chini ya Ufalme mwadilifu wa Mungu.”
2 Wakati wa Novemba tutaelekeza uangalifu wa pekee kwa fungu ambalo Neno la Mungu, Biblia, hutimiza katika kusaidia watu kukabiliana na misongo itokayo ulimwenguni. Tutatoa New World Translation of the Holy Scriptures na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Ni nini tuwezacho kusema kitakachosaidia watu mmoja-mmoja wenye mtazamo ufaao ili wathamini thamani ya Biblia?
3 Baada ya kujijulisha, unaweza kusema jambo kama hili:
◼ “Yamkini utakubali kwamba tunazungukwa na matatizo yanayoelekea kutunyang’anya amani yetu ya akili. Twaweza kupata wapi shauri lenye kutumika la kutuonyesha jinsi ya kukabiliana na matatizo haya? [Ruhusu itikio.] Nimeona Biblia kuwa yenye kutuhakikishia kwa sababu hiyo hutufundisha jinsi ya kuwa wenye furaha. [Soma Luka 11:28.] Kusudi la kazi yetu ni kuwatia watu moyo wasome Biblia na kunufaika kutokana na maagizo yayo. Msaada huu wa kujifunza Biblia, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, waweza kukusaidia ufanye hivyo. Ona jinsi kinavyosema juu ya chanzo cha matatizo yaliyo mengi ya ulimwengu.” Soma mstari wa pili wa fungu la 9 kwenye ukurasa 187. Hata unaweza kumalizia na Yeremia 17:9 kabla ya kutoa toleo.
4 Unaweza kuchagua kutumia mfikio sahili kama huu:
◼ “Tunapendezwa kutia moyo kuwa na heshima kubwa kwa Neno la Mungu, Biblia. Ningependa kukupa nakala ya trakti hii, Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia. Hii hueleza sababu tunayoweza kuitazama Biblia ili tupate tumaini hakika kwa ulimwengu bora. [Fungua ukurasa 6, na usome Zaburi 37:29 pamoja na fungu la kumalizia.] Jisomee mwenyewe trakti hii, na nikikutembelea wakati ujao, acha nijue unalofikiri juu ya tumaini ambalo Biblia hutoa.”
5 Wahubiri fulani huenda wakataka kutumia mfikio huu wa moja kwa moja wa kuanzisha funzo la Biblia:
◼ “Ninazuru ili nikutolee mtaala wa funzo la Biblia nyumbani bila malipo. Biblia imepuliziwa na Mungu, na maagizo yayo yaweza kutusaidia turekebishe mambo. Hii New World Translation of the Holy Scriptures yenye lugha ya kisasa imefanyizwa kwa ajili ya funzo la kibinafsi. Imethibitika kuwa yenye kupendwa na mamilioni ya wasomaji wa Biblia ulimwenguni pote. Acha nikuonyeshe kifupi jinsi unavyoweza kuitumia. [Fungua ukurasa 1653, na uelekeze uangalifu kwa 23A. Fungua andiko moja au mawili yaliyowekwa bila manukuu na uzungumzie jambo linalotajwa hapo. Eleza jinsi kutazama maandiko yaliyowekwa bila manukuu kutaonyesha yale Mungu amekusudia kutimiza kupitia Ufalme wake.] Ningependa kurudi ili tuzungumze juu ya tumaini hili la Ufalme zaidi.”
6 Biblia ni chanzo cha faraja na tumaini pamoja na kweli inayoweza kutuongoza kwenye uhai wa milele. (Yn. 17:3, 17) Kushiriki ujuzi wa Biblia pamoja na wengine humpendeza Yehova, “ambaye hutaka watu wote waokolewe.”—1 Tim. 2:4.