Wasaidie Wasikie “Tena”
1 “Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.” (Mdo. 17:32) Hilo ndilo lilikuwa itikio la watu fulani kwa hotuba inayojulikana sana ya Paulo kwenye Kilima Mars. Vivyo hivyo leo, watu fulani wana nia ya kusikiliza zaidi kuhusu ujumbe wa Ufalme ambao tulishiriki pamoja nao katika ziara yetu ya kwanza.
2 Sisi hufanya kiwango kikubwa cha kuhubiri kwetu tunaporudi kusitawisha kupendezwa. Utayarishaji mzuri utatusaidia tupate matokeo mazuri. Ukurasa 51 wa kitabu Kiongozi cha Shule hupendekeza: “Kwanza zifahamu waziwazi hoja zenye kuthibitisha habari. Jaribu kujua ni kwa sababu gani jambo liko vile. Hakikisha uone ikiwa unaweza kuyatia mawazo katika maneno yako mwenyewe. Pata ufahamu mzuri wa uthibitisho wa Maandiko. Uwe tayari kuyatumia maandiko kwa kufaa.”
3 Ikiwa uliangusha kitabu “Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?,” unaweza kusema jambo kama hili:
◼ “Tulipoongea wakati uliopita, tulizungumzia sababu kwa nini tunaweza kuwa na uhakika katika Biblia. Kitabu nilichokuachia chatokeza lile swali: ‘Kwa Nini Uisome Biblia?’ [Soma utangulizi kwenye ukurasa 5, na uruhusu itikio kwa swali la kumalizia.] Biblia yatuambia kwamba hivi karibuni Mungu mwenyewe atatatua matatizo yote yenye kutatiza ya wanadamu, nayo huongoza katika njia tunayopaswa kwenda ili tufurahie baraka za wakati huo wenye furaha. [Soma Zaburi 119:105.] Kitabu hiki kimetengenezwa kiwe msaada wa funzo la Biblia la kibinafsi na la familia. Nitafurahi kukuonyesha jinsi ya kukitumia.”
4 Kwenye ziara ulizoacha trakti “Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia,” unaweza kusema hivi:
◼ “Sisi sote tunapendezwa na yale yatakayotokea wakati ujao. Kwa sababu ya hali za ulimwengu wa sasa, unafikiri ni nini litakalotokea? [Ruhusu itikio.] Ijapokuwa mwanadamu anaweza tu kudhania-dhania kuhusu yatakayotokea, Mungu anajua ni nini hasa litakalotokea. [Soma Isaya 46:10.] Huenda ukashangaa kujua kwamba Biblia hutabiri kwamba karibuni tutafurahia baraka za paradiso ya ulimwengu mpya. [Soma fungu la tatu kwenye ukurasa 4.] Acha nikuambie mengi zaidi kuhusu ahadi hii nzuri ajabu.”
5 Ikiwa unafuatia angusho la “New World Translation,” labda dokezo hili litakuwa lenye matokeo kwako:
◼ “Hivi majuzi, nilikuachia nakala ya Biblia, nami niliahidi kurudi nikusaidie ukitumie kwa manufaa. Wakati mwingine huenda tukashangaa jinsi tunavyoweza kusitawisha mahusiano ya kirafiki pamoja na wengine. Biblia ina shauri zuri la kutoa, na New World Translation hufanya iwe rahisi kupata tunachohitaji. [Fungua ukurasa 1595 na utazame chini ya kichwa “Upendo.” Toa uangalifu kwa maandiko kama vile 1 Wakorintho 13:4; Wakolosai 3:14; na 1 Petro 4:8. Elezea kifupi jinsi kutumia kanuni hizi kunavyoweza kuleta matokeo mazuri.] Huu ni mfano mmoja wa kuonyesha jinsi Biblia hutoa utatuzi wenye kutumika kwa matatizo yetu. Wakati ujao, ningependa kukuonyesha njia nyingine ambayo Biblia inaweza kutusaidia tupate furaha na amani ya akili.”
6 Hakuna hazina kubwa zaidi tuwezayo kupitishia wengine kuliko ujuzi sahihi wa Neno la Mungu. Ujuzi huo waweza kufundisha hofu ya Yehova na kuwatia watu moyo watembee katika njia yake, ambayo huleta baraka za milele.—Mit. 2:20, 21.