Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/89 kur. 3-4
  • Kwenda Sambamba na Ongezeko la Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwenda Sambamba na Ongezeko la Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUNA MENGI ZAIDI YA KUFANYA
  • MICHANGO INATHAMINIWA KIKWELI
  • Kudhihirisha Imani kwa Matendo Mema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Upanuzi Wenye Kuendelea Waongeza Uhitaji wa Majumba ya Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Fungu Lako Katika Kujenga kwa Ajili ya Wakati Ujao
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Afrika Mashariki
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 12/89 kur. 3-4

Kwenda Sambamba na Ongezeko la Kitheokrasi

1 Katika siku ya Nehemia, kulikuwako uhitaji wa ujenzi kwa sababu kuta za kinga za Yerusalemu zilikuwa magofu. Nehemia alitoa uongozi wenye kukata maneno, na watu waliitikia, wakisema, “Haya! na tuondoke tukajenge.”—Neh. 2:18.

2 Leo, hali moja na hiyo, watu wa Yehova wanaitikia uhitaji wa kujenga na kurekebisha Majumba ya Ufalme. Mamia ya Majumba ya Ufalme yanahitaji sana kurekebishwa, na mamia ya majumba mapya yanahitaji kujengwa ili kutoa nafasi kwa upanuzi wa haraka sana wa tengenezo la Yehova. Sawa na vile Nehemia alivyopanga kitengenezo kazi ya kujenga upya kuta za Yerusalemu, ndivyo “mtumwa mwaminifu na mwenye akili” amepanga kitengenezo programu ya ujenzi leo kwa kuanzisha katika maeneo fulani Hazina ya Sosaiti ya Jumba la Ufalme na kuweka Halmashauri za Ujenzi za Majimbo.—Mt. 24:45.

3 Ingawa katika eneo letu mpango wa Hazina ya Sosaiti ya Jumba la Ufalme haupo tunafurahi kujua Sosaiti imetegemeza ujenzi wa Majumba ya Ufalme mapya ya makundi kadha kupitia mikopo. Kufikia sasa makundi 19 katika eneo la Afrika Mashariki yamepokea mikopo kutoka kwa Sosaiti ili kujenga Jumba la Ufalme na mengine kadhaa tayari yamepeleka maombi yao ya msaada huo. Hiyo haitii makundi ambayo wakati uliopita yamekopa pesa kwa makusudi ya ujenzi na ambayo kufikia sasa yamekwisha kujenga Majumba ya Ufalme yao na kulipia mikopo yao katika kipindi kilichoafikiwa. Michango ya ukarimu ya akina ndugu imewezesha Sosaiti isaidie makundi kwa kuyapa mikopo ya ujenzi wa Jumba la Ufalme. Itikio hilo la kutegemeza ongezeko la kitheokrasi limekuwa lenye kuchangamsha moyo.—1 The. 4:9, 10.

4 Pia katika eneo letu hatuna Halmashauri za Ujenzi za Majimbo lakini Sosaiti imetoa miongozo fulani ya kusaidia katika kuchora ramani ya Jumba la Ufalme lenye kiasi na lenye kufaa na litakalotumia kwa hekima vifaa vilivyokwisha kutolewa. Ndugu wengine wamejitolea kusaidia katika kuchora ramani za jengo zitumiwe kwa ujenzi. Wengine wamejitolea ustadi na utaalamu wao wa kujenga na kusafiri masafa marefu ili wasaidie makundi na kazi zayo za ujenzi. Kuhusiana na kazi yoyote ya ujenzi baraza la wazee litapima mambo yote kwa uangalifu kutia fedha zilizopo, ramani zenye kiasi, na maoni ya akina ndugu wanaosaidia kazi zao za ujenzi.—Luka 14:28-30.

KUNA MENGI ZAIDI YA KUFANYA

5 Ingawa Majumba ya Ufalme mengi yamekwisha kujengwa, kuna mengi zaidi ya kutimizwa ili kwenda sambamba na ongezeko la kitheokrasi. Mengine ya Majumba ya Ufalme yaliyojengwa karibuni tayari yana makundi kadhaa yanayokutania humo. Hiyo maana yake ni kwamba karibuni jumba jingine litahitajiwa ili kutoa nafasi kwa ajili ya ukuzi katika maeneo hayo. Makundi mengine yanasubiri fedha zipatikane ili kutimiza mahitaji ya wakati huu. Kwa wazi utegemezaji wetu wenye kuendelea wa kazi ya Ufalme unahitajiwa.

6 Inapatana na Maandiko kutoa utegemezo za kifedha. Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “mchango” linamaanisha “fungu takatifu.” (Kut. 25:2, Reference Bible, kielezi cha chini) Kwa usahihi Wakristo wanatamani kuchanga wakati wao, nishati, na mali zao za kimwili ili kusogeza mbele masilahi ya Ufalme. Hatumtajirishi Yehova na michango yetu tunayotoa kwa kazi yake, lakini kwa njia hiyo tunaonyesha upendo wetu kwake, naye hubariki wale wanaochanga kwa kujitolea.—1 Nya. 29:14-17; Mit. 3:9.

7 Paulo aliandika hivi kwenye 2 Wakorintho 8:12: “Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri asivyo navyo.” Wote wanaweza kutiwa moyo waweke kitu fulani kando kwa ukawaida kulingana na uwezo na tamaa yao. (Linganisha 1 Wakorintho 16:1-4.) Tertuliano aliandika hivi juu ya kundi la kwanza la Kikristo: “Kila mtu mara moja kwa mwezi huleta sarufi ndogo—au wakati wowote apendapo, na ikiwa tu anataka, na kama anaweza; kwa maana hakuna anayelazimishwa; ni toleo la kujitolea.” Tofauti na dini nyingi leo zinazopitisha sahani ya kuchangisha ili kudai michango, matoleo yote ya kimwili katika kundi la Kikristo yanayotolewa kwa kujitolea kutoka moyoni. (2 Kor. 9:7) Kuhusu hilo makundi na mizunguko mingi imesaidia kwa ukawaida kwa kupitisha maazimio yanayotoa idhini fedha zichangwe kwa Sosaiti. Watu mmoja mmoja wanaopenda kufanya hivyo wanaweza kutoa michango ya kujitolea kwa Sosaiti. Majibu ya michango ya wakati uliopita yanaposomewa kundi, wote wanakumbushwa juu ya ushiriki ambao wao binafsi wanaweza kuwa nao.

MICHANGO INATHAMINIWA KIKWELI

8 Utegemezo wetu wenye kuendelea wa kazi ya Ufalme tukiwa mizunguko, makundi, na watu mmoja mmoja inahitajiwa sana ili kwenda sambamba na ongezeko la kitheokrasi. Utegemezo wenu wa ukarimu na wakati na ustadi wa kujitolea wa wengi ambao wamesaidia katika ujenzi na kurekebisha Majumba ya Ufalme vinathaminiwa kwa moyo mweupe. Hata hivyo, kuna uhitaji wa kuharakisha mwendo wetu tutimize uhitaji wa Majumba ya Ufalme zaidi.

9 Kundi moja liliandika hivi: ‘Tunataka kuwashukuru nyinyi akina ndugu kwa kutuonyesha imani na utumainifu kwa kutukopesha pesa za kugharimia kazi yetu. Kuongezea hayo, tungependa kuwashukuru kwa ajili ya Halmashauri za Ujenzi za Majimbo, nasi kwa moyo mweupe tunathamini ndugu wenye vipawa waliotumiwa kuhusiana na kazi yetu ya ujenzi.’

10 Kundi jingine lilisema: ‘Tulipofanyiza kikundi kilicho peke yake katika Mei 1985, tulianza kukutana katika nyumba ya dada mmoja. Wengi wa ndugu waliobatizwa walisimama kwenye mikutano. Hudhurio letu lilipoendelea kuongezeka, kukawa hakuna nafasi hata ya kusimama. Kundi lingependa kupeleka shukrani zalo za kutoka moyoni kwenu ndugu kwa ajili ya kuchukua hatua haraka na kupendezwa na mahitaji yetu. Hilo pia lilikuwa ni baraka kutoka kwa Yehova katika kujibu sala zetu. Kundi limesisimuka we! kuwa ndani ya Jumba la Ufalme jipya hili.’

11 Tuna maandishi ya yale yaliyotimizwa katika siku ya Nehemia. Ujapokuwa upinzani kutoka kwa mataifa adui, Waisraeli walifuata uongozi wa moyo mkuu wa Nehemia, na kwa baraka ya Yehova walikamilisha kuta za Yerusalemu kwa siku 52 peke yake. Nehemia 4:6 inasema “watu walikuwa na moyo wa kufanya kazi.” Kwa hiyo leo, chini ya uelekezo wa mtumwa mwaminifu na mwenye akili, kazi kubwa ya ujenzi inatimizwa, na tengenezo la ki-siku-hizi la Yehova ‘limeendelea kuwa na moyo wa kufanya kazi.’ Tunajiunga nanyi katika kusali tupate baraka tele za Yehova tunapojitahidi kwenda sambamba na ongezeko la kitheokrasi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki