Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/90 kur. 3-4
  • Wakati wa Utendaji Ulioongezwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakati wa Utendaji Ulioongezwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • SHEREHE YA UKUMBUSHO NA HOTUBA YA PEKEE
  • ONGEZA UGAWANYAJI WA MAGAZETI BORA
  • Je! Aprili Utakuwa Mwezi wa Pekee Kwako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • ‘Lihubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Majira ya Ukumbusho—Fursa ya Kuongeza Utendaji!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Iweni Wenye Bidii kwa Lililo Jema!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 3/90 kur. 3-4

Wakati wa Utendaji Ulioongezwa

1 Mwisho wa huu mfumo wa mambo uliopo ukaribiapo na sisi kuona jinsi Yehova anavyobariki sana huduma yetu, hatuna budi kutii shauri la mtume Petro ‘kufunga viuno vya akili zetu kwa ajili ya utendaji.’—1 Pet. 1:13, NW; Isa. 60:22.

2 Wakati Petro alipotoa shauri lililo juu, alikuwa akiandika juu ya wokovu unaoweza kuwa wetu kupitia damu iliyomwagwa ya Yesu Kristo. Kutangaza kwetu habari njema za Ufalme ni njia moja ya maana tuliyo nayo ya kudhihirisha imani yetu na kuonyesha uthamini wetu kwa ajili ya baraka tunazopokea kwa sababu ya upendo wa Yehova unaoonyeshwa kupitia zawadi ya Mwanaye. (Yn. 3:16) Majira ya Ukumbusho ni wakati wa kuwa wenye kutenda hata zaidi katika kazi hii iliyoagizwa rasmi na Mungu.

SHEREHE YA UKUMBUSHO NA HOTUBA YA PEKEE

3 Sherehe ya Ukumbusho mwaka huu itafanywa baada ya jua kutua mnamo Aprili 10. Hata sasa, katika kutarajia tarehe hiyo ya pekee, tunaweza kuchunguza uhusiano wetu pamoja na Yehova Mungu na jinsi tunavyokumbuka dhabihu ya Yesu. Je! sisi tunadhihirisha imani yetu kila siku kwa kushikamana sana na viwango vya uadilifu vya Yehova katika kufikiri kwetu, usemi, na mwenendo? Je! sisi tunaonyesha wengine upendo kwa kujitahidi katika kuhubiri juu ya Ufalme na katika kufanya wanafunzi? Kwa njia ya pekee kila mwaka kwenye sherehe ya Ukumbusho, tunakumbuka yale ambayo Yehova Mungu na Yesu wametufanyia sisi. (Luka 22:19; 1 Kor. 11:23, 24) Ukumbuko huo wa kutafakari wapasa kutuchochea tutende kwa uchanya kulingana na uwezo na mastakimu zetu za kibinafsi.

4 Mnamo Machi 25, makundi yaliyo mengi ya Mashahidi wa Yehova kuuzunguka ulimwengu yatatoa hotuba ya pekee juu ya habari hii “Jitahidi Kufikia Uzima Ulio Kweli Kweli!” Ni fursa nzuri kama nini kwa wapya kuanza kushirikiana na kundi! Wale watakaohudhuria hotuba ya pekee wapasa kutiwa moyo wawepo kwa ajili ya sherehe ya Ukumbusho mnamo Aprili 10.

ONGEZA UGAWANYAJI WA MAGAZETI BORA

5 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanatimiza fungu la muhimu katika huduma yetu ya peupe huku yakiandaa chakula cha kiroho na usomaji wa wakati wake kwa ajili yetu sisi sote. Wahubiri wote wa Ufalme watathamini jitihada ya pekee ambayo imefanywa katika kutayarisha magazeti hayo kwa ajili ya Machi, Aprili na Mei. Tutakuwa tukikazia matoleo hayo tutoapo maandikisho. Jitahidi kuzoeleana kabisa na kila toleo mara tu ulipokeapo. Kufanya hivyo kutachochea bidii yako kwa ajili ya kulitoa shambani utoapo maandikisho na nakala moja moja au utoapo magazeti mawili pamoja na mojawapo broshua kwa wale wasioandikisha.

6 Katika ratiba yako ya kibinafsi, je! unaweza kuutafutia nafasi upainia msaidizi wakati wa Aprili na Mei? Ikiwa wahubiri kadhaa katika kundi wanapanga kupainia wakati ule ule, wanaweza kusaidiana na kutiana moyo wakati wa kipindi hiki cha pekee cha utendaji ulioongezwa. Wazee watapendezwa kusaidia kwa kufanya mipango ya ziada kwa ajili ya utoaji wa ushahidi wa kikundi inapokuwa lazima.

7 Fikiria kwa uzito juu ya mastakimu zako, kama vile madaraka ya jamaa, afya ya kimwili, kazi ya kimwili, au ratiba ya shule. Usipoweza kupainia wakati huo, ni kwa kadiri gani unaweza kuongeza ushiriki wako katika huduma ya shambani? Hakika Yehova anapendezwa na utumishi wa nafsi yote unaoonyesha upendo na uthamini wetu kwa ajili yake na kwa ajili ya zawadi ya thamani ya Mwanaye, Yesu. Tujichunguzapo wenyewe kwa msaada wa Neno la Mungu na kufunga viuno vya akili zetu kwa ajili ya utendaji, tunaweza kuwa na uhakika wa kuwa na roho ya Yehova ikitutegemeza katika kutoa dhabihu za sifa zenye kukubalika.—Ebr. 13:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki