Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/90 uku. 1
  • Shiriki Utajiri wa Kiroho Pamoja na Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shiriki Utajiri wa Kiroho Pamoja na Wengine
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI YA KUTAJIRISHA WENGINE
  • Kuazimia Kuwa Tajiri Kiroho
    Amkeni!—2007
  • ‘Tukiwa Hatuna Kitu Lakini Tukiwa na Vitu Vyote’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Unaweza Kupata Utajiri!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Tumaini Lako—Je, Ni Mungu au Mali?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 5/90 uku. 1

Shiriki Utajiri wa Kiroho Pamoja na Wengine

1 Kama vile Musa mwaminifu, Mashahidi wa Yehova wa ki-siku-hizi wanajua kwamba hazina za kimwili za ulimwengu huu haziwezi kulingana thamani na utajiri wa kiroho. (Ebr. 11:26) Fedha zaweza kununua nyumba, motokaa, na mali nyinginezo, lakini haziwezi kununua uhai, amani ya akili, au kibali na baraka za Yehova Mungu.

2 Maarifa na uelewevu wa Neno na kusudi la Mungu ni utajiri halisi wa kiroho. (Kol. 2:3) Utajiri huu wa pekee waweza kuleta furaha ya kweli sasa, pamoja na tumaini hakika la wakati ujao. Jinsi sisi tulivyopendelewa kwa kupokea utajiri huo!

JINSI YA KUTAJIRISHA WENGINE

3 Twaweza kusaidia wengine wengi watajirike kiroho kwa kuwajulisha Mnara wa Mlinzi, kwa kuwa laweza kuwaongoza kwenye “hazina iliyositirika” ya hekima ya kimungu. (Mit. 2:4) Wakati wa Mei, tutatoa andikisho la Mnara wa Mlinzi kwenye kila pindi inayofaa. Tukikumbuka jinsi Mnara wa Mlinzi umetajirisha maisha zetu, hatutasita bali tutatafuta njia za kulitoa kwa watu wengi tuwezavyo. (Mit. 3:27) Andika anwani ambako magazeti na broshua moja moja zinaangushwa, ukiwa na kusudi la kufuatia na kusitawisha kupendezwa kokote kulikoonyeshwa.

4 Katika maana ya kiroho, sisi twawezaje kuwa kama yule mtu mwenye kuhofu Mungu wa Zaburi 112 aliyegawanya sana vitu vyake vya thamani? (Zab. 112:1, 3, 9) Twahitaji kuwatafuta wenye mfano wa kondoo na kuwasaidia wajaze uhitaji wao wa kiroho. (Mt. 5:3) Hilo lataka kwamba tutumie kwa faida kila fursa kutoa ushahidi uliopangwa na wa vivi hivi.

5 Katika maeneo fulani, ushahidi wa jioni umekuwa wenye mazao sana kwa sababu watu zaidi waelekea kuwa nyumbani wakati huo. Je! wewe umepata kujaribu kufanya kazi mlango kwa mlango kwa saa moja hivi au kabla ya Funzo la Kitabu la Kundi au jioni nyingine wakati wa juma? Kwa nini usifanye mipango kamili ya kufanya hivyo? Huenda kufanya hivyo kukathibitika kuwa kwa kuthawabisha sana kwako.

6 Je! waweza kupata nyakati zinazofaa za kutoa ushahidi mahali pako pa kazi? Dada mmoja aliwekelea magazeti kadhaa kwenye deski yake ili kwamba wafanya kazi wenzake waweze kuona walipokuwa wakipita. Kabla ya asubuhi kwisha, magazeti yote yalikuwa yameangushwa. Hesabu kubwa ya wafanya kazi wenzake walionyesha upendezi halisi, naye aliweza kuangusha maandikisho 18.

7 Fedha, dhahabu, na hazina nyinginezo zote za kimwili haziwezi kulingana na utajiri wa kiroho wa maarifa na uelewevu ambao tumepata kupitia tengenezo la Yehova na kupitia funzo letu la Biblia. Furaha halisi, njia za kupendeza, amani, “wingi wa siku”—hata uhai wa milele—vyote vyawezekana kwa wale wanaotafuta utajiri wa kiroho. (Mit. 3:13-18) Kwa kushiriki utajiri wetu wa kiroho pamoja na wengine, twaonyesha uthamini kwa ajili ya yale tuliyopokea na twapata baraka ya Yehova yenye kuendelea.—Mit. 19:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki