Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/90 kur. 7-8
  • Je! Watoto Wako Ni Tayari Kurudi Shuleni?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Watoto Wako Ni Tayari Kurudi Shuleni?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUMIENI BROSHUA SHULE
  • UWE SHAHIDI KILA SIKU
  • Kushirikiana na Mfumo wa Shule
    Shule na Mashahidi wa Yehova
  • Funguo za Elimu Nzuri
    Amkeni!—1995
  • Kurudi Shuleni Tena
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Vijana—Tumieni kwa Manufaa Masomo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 8/90 kur. 7-8

Je! Watoto Wako Ni Tayari Kurudi Shuleni?

1 Baada ya majuma machache tu, vijana Wakristo watarudi shuleni. Huenda hilo likawa ni pamoja na kadiri fulani ya msisimuko na yawezekana wasiwasi fulani. Hisia hizo za ndani hutokezwa na fursa na matatizo yanayotazamiwa. Baadhi ya vijana watakutana na wanadarasa wenzi na walimu wapya. Vijana Wakristo hutambua pia kwamba kila muhula mpya wa shule huambatana na mitihani ya imani yao, ukamilifu, na upendo kwa ajili ya Yehova. Je! nyie wachanga kundini mko tayari kurudi shuleni? Nyinyi wazazi mwaweza kuimarishaje watoto wenu kwa ajili ya mitihani iliyo mbele?

TUMIENI BROSHUA SHULE

2 Katika 1983 broshua Shule iliandaliwa hasa kwa ajili ya wazazi Wakristo na watoto wao wenye umri wa kwenda shuleni. Imekusudiwa isaidie kutokeza waziwazi kwa walimu na wasimamizi imani na mazoea ya Mashahidi wa Yehova kwa kuwa zinahusiana na utendaji fulanifulani wa shule. Pia huandaa miongozo juu ya msimamo wenye umoja wa Mashahidi wa Yehova kuhusiana na staha kwa mwenendo wa adili.

3 Kwa vijana wengi broshua hii imethibitika kuwa himaya kweli kweli. Kwa kielelezo, mzazi mmoja Shahidi alipata kujua kwamba hotuba za elimu ya ngono zingetolewa wanafunzi na watu waliojulikana kuwa walioachilia adili. Akiwa na broshua hiyo, mzazi huyo aliweza kuzungumza makatao yake ya Kimaandiko na akafaulu kufanya mabadiliko yanayofaa katika masomo ya bintiye.

4 Kabla ya shule kuanza, wazazi wanaweza kuimarisha akili na mioyo ya watoto wao kwa kuchukua wakati kuburudisha kumbukumbu zao na yaliyomo katika broshua hiyo. Kwa ufikirio unaofaa wa umri wa watoto, darasa, na shule, wazazi waweza kukazia mawazo bora kutoka broshua hiyo yanayoweza hasa kuwa msaada katika mwaka. (Mit. 14:15; 22:3) Fanya mazoezi na mtoto wako juu ya hali zinazoweza kumkabili, na udhihirishe jinsi habari iliyochapishwa inavyoweza kunufaisha katika ‘kufanya vijia vilivyonyooka kwa ajili ya nyayo zake.’—Ebr. 12:13, NW.

5 Wazazi wanaweza kufanya mengi kuwasaidia watoto wao “kujitetea mbele ya kila mtu” anayeweza kuwasaili juu ya maoni yao ya kibinafsi na matumaini. (1 Pet. 3:15, NW) Katika visa fulani wazazi wanaweza kuchagua kuongea kibinafsi na mwalimu. Baadhi ya wazazi Wakristo huratibu ziara za pindi kwa pindi za kwenda shuleni, kwa kuwa jambo hilo laweza kusaidia kufanyiza uhusiano mzuri baina yao na walimu. Upendezi huo wa kibinafsi pia hutia nguvu uhusiano baina ya mzazi na mtoto. Nyakati nyingine hilo humpa mzazi hisia halisi ya mazingira na misongo ya kipekee ya siku kwa siku wanayokabili watoto wetu.—1 Pet. 3:8.

UWE SHAHIDI KILA SIKU

6 Shahidi mmoja kijana katika Kolorado alikuwa akimwuliza mwalimu wake amsaidie kuelewa maneno magumu aliyokuta akisoma kijitabu Kuyachunguza Maandiko kila siku. Siku moja akatambua kwamba kijitabu chake hakipo. Baadaye alipata kwamba mwalimu wake alikuwa “ameiazima” siku aliyotoka shuleni mapema kwa sababu alikuwa mgonjwa. Yeye hakutaka kukosa kusoma andiko. Hilo liliongoza kwenye kumwandalia nakala yake mwenyewe ya Kuyachunguza Maandiko.

7 Ni kweli kwamba muhula mpya wa shule hutokeza pindi za wasiwasi na hangaiko. Hata hivyo, maoni chanya pamoja na matayarisho yenye juhudi yatasaidia wazazi na vijana ‘kufunga viuno vya nia zao’ iwe kwa sifa ya Yehova wakati wa muhula ujao wa shule.—1 Pet. 1:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki