Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/90 kur. 1-12
  • Fikia Mioyo Kupitia Mafunzo ya Biblia Yenye Mafanikio

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fikia Mioyo Kupitia Mafunzo ya Biblia Yenye Mafanikio
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KAZIA BIBLIA
  • ULIZA MASWALI
  • Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Kutumia Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kazia Uangalifu ‘Ufundi Wako wa Kufundisha’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Fikia Moyo wa Mwanafunzi Wako wa Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 10/90 kur. 1-12

Fikia Mioyo Kupitia Mafunzo ya Biblia Yenye Mafanikio

1 Yesu alipata furaha katika kufanya mapenzi ya Baba yake, naye alifurahia kusaidia wengine pia wamtumikie Yehova. (Zab. 40:8; Mt. 9:37, 38; 11:28-30) Yesu hakuridhika tu na kutoa ujumbe wake. Ikiwa tutafanikiwa katika kutia wengine moyo wajiunge nasi katika kazi ya kueneza evanjeli, lazima sisi tufikie mioyo ya wanafunzi wetu wa Biblia. Hiyo inahusu zaidi ya kuongoza mazungumzo ya maswali na majibu ya kichapo. Ili kufikia moyo, twahitaji kujitayarisha kwa kumfikiria mwanafunzi wetu.

2 Yesu alipendezwa kibinafsi na wengine. Alifikiria maoni yao. Alitumia vielezi ili kufanya somo gumu liwe sahili. (Mt., Sura 5-7) Akifahamu magumu ambayo wangekabili, Yesu aliwapa ushauri unaofaa. (Mk. 9:33-37) Wakati wasikilizaji wake waliposhindwa mwanzoni kufahamu maana ya fundisho lake, alitoa kwa saburi kielezi cha yale aliyotaka kusema. (Mt. 16:5-12) Kupendezwa kwa kina kirefu kwa Yesu na wengine kwapasa kutusukume tujiulize, ‘Kama mimi ningekuwa ndiye mwanafunzi, ningehitaji kujua nini ili kuelewa na kusukumwa na yale yanayofundishwa?’—Angalia Kitabu-Mwaka 1971 (Kiingereza) kurasa 246-7.

KAZIA BIBLIA

3 Wakati wenzi wa ndoa walipoulizwa ni nini kilichowafanya waitikie kwa utayari sana ushahidi uliotolewa, walijibu: “Ulikuwa katika Biblia.” Ndiyo, Neno la Mungu hufikia mioyo. (Ebr. 4:12) Lirejezee mara nyingi, ukitumia kwa wingi maandiko yaliyo katika mafungu. Saidia mwanafunzi aone kwa nini mwendo fulani ni wa hekima au wa upumbavu. Sababu naye juu ya jinsi utii kwa sheria za Mungu utamnufaisha.—Ona Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1985, kurasa 19-20.

4 Wahubiri wengi wamepata kwamba kutumia kitabu Kutoa Sababu kuna mafanikio sana katika kukazia Biblia. Kwa kielelezo, wanapozungumza ukurasa 124, fungu la 13, la kitabu Kuishi Milele huenda mwenye nyumba akauliza kwa nini padri wake husema kwamba watoto hufa kwa sababu Mungu ataka wawe pamoja naye mbinguni. Mazungumzo ya habari kwenye ukurasa 101 wa kitabu Kutoa Sababu chini ya “Kwa nini vitoto vichanga vinakufa?” hukazia kwamba Yehova hupendezwa na kuhifadhiwa kwa mpango wa familia. Huenda habari hiyo ikamsadikisha mtu huyo juu ya upendo wa Yehova kwa ainabinadamu.

ULIZA MASWALI

5 Utumizi wa maswali wenye mafanikio ulimsaidia Yesu awafanye watu wafikiri na kusababu. (Mt. 17:24-27) Majibu ya mwanafunzi yaweza kutusaidia tuamue yale anayojifunza pamoja na maoni yasiyo ya Kimaandiko ambayo angali anashikilia. Labda mwanafunzi apiga vita dhidi ya zoea la kuvuta sigareti. Mmepitia habari katika sura ya 27 ya kitabu Kuishi Milele na habari katika kurasa 13-16 katika Machi 8, 1990, toleo la Amkeni! Aona uhitaji wa kuacha. Lakini je! yeye anasadikishwa kikweli kwamba apaswa kuacha kabisa awe huru nalo? Waweza kusema: “Wewe wahisije juu ya jambo hili? Tuseme ungeacha sasa hivi lakini baadhi ya marafiki wako wakucheke. Wewe ungefanyaje?”

6 Ingawa hivyo, pana neno la kukutahadharisha. Nyakati nyingine maswali kama hayo huenda yakaleta majibu yanayoweza kukushangaza au kukutamausha. Iweje? Ikiwa ni habari inayoweza kuudhi kwa vyepesi, ingekuwa afadhali kutofuatilia sana swala hilo lakini useme: “Acha tuendelee kwa sasa. Twaweza kulirudia baadaye.” Au “Basi, ni jambo la kufikiria, sivyo?” (Yn. 16:12) Ukijua vile mwanafunzi anavyohisi kikweli juu ya jambo hilo, waweza kutayarisha habari ambayo huenda ikamsaidia kufanya maendeleo zaidi. Twapaswa kujitahidi kuchochea moyo wa mtu na kusali kwamba Yehova atamsaidia akue kiroho.—1 Kor. 3:5-9.

7 Unapoongoza funzo la Biblia, kumbuka sikuzote kutumia wakati wa kutosha kusababu na mwanafunzi juu ya habari inayozungumzwa. Patanisha njia zako za kufundisha zifaane na mahitaji yake hususa. Fanyia kazi kujenga ndani ya moyo wake upendo na staha yenye kina kwa Yehova, Biblia, na tengenezo la Yehova. Sisi na tufanye sehemu yetu katika kusaidia wengine wawe wanafunzi wa Kristo kwa kujaribu kuongoza mafunzo ya Biblia yenye mafanikio.—Mdo. 2:41-46.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki