Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
ANGALIA: Huduma ya Ufalme Yetu itaratibu Mikutano ya Utumishi kwa kila juma wakati wa miezi ya Mkusanyiko. Makundi yanaweza kufanya marekebisho kama inavyohitajiwa ili kuruhusu wakati wa kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya halafu kuwe na pitio la dakika 30 kuhusu mambo makuu ya programu kwenye Mkutano wa Utumishi juma linalofuata. Pitio la siku baada ya siku linaweza kugawiwa mapema ndugu wawili au watatu wanaostahili ambao wataweza kukazia mambo ya msingi. Pitio hili lililotayarishwa vizuri litasaidia akina ndugu wakumbuke mambo ya msingi ili wayatumie kibinafsi na shambani. Mambo yaliyoonwa yanayotumiwa na maelezo kutoka kwa wasikilizaji yanapaswa kuwa mafupi na kutokeza wazo kuu.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Dokeza namna mbili za kutoa Amkeni! ambazo zingefaa katika eneo lenu.
Dak. 17: “Endelea Kufundisha Bila Kuacha.” Mazungumzo na maonyesho. Baada ya kuzungumza fungu la 2, mapainia au wahubiri mwenye mafanikio watoe wonyesho wa jinsi ya kutoa uandikishaji kwa mtu anayeonyesha kupendezwa halisi katika ujumbe wa Ufalme. Ikiwa mtu huyo angependa kupokea gazeti (magazeti) kwa ukawaida, tutafurahia kumwandikisha ili awe akipata magazeti kupitia sanduku lake la posta. Baada ya fungu la 3 na 4, wahubiri wawili wenye idili wazungumze jinsi watakavyotumia madokezo hayo wakati wa Oktoba na katika miezi ijayo.
Dak. 18: “Fikia Mioyo Kupitia Mafunzo ya Biblia Yenye Mafanikio.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya makala hiyo. Wakati wa kuzungumzia fungu la 3 na 5, toa wonyesho wa kujipatanisha na hali za kwenu. Kazia mambo yanayofaa katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1985.
Wimbo 195 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 8
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: Wazazi Msiwe Mkiwaudhi Watoto Wenu. Hotuba na wonyesho ikitegemea kurasa 16 na 17 za Amkeni! (Kiingereza), Januari 22, 1990 (au Amkeni! Novemba 8, 1990 makala “Kupitia Macho ya Watoto”), na vichwa vidogo “Kumtia Moyo Mtoto Wako Awe Akisema” na “Kufahamu Mahitaji ya Watoto Wenye Umri wa Kati ya Miaka 13 na 19” katika sura ya 11 ya kitabu Maisha ya Jamaa. Kazia uhitaji wa wazazi kufahamu kila mmoja wa watoto wao na kuwasaidia wakue kiroho na vinginevyo. Mwishoni mwa funzo la Biblia, toa wonyesho wa jinsi mzazi hupongeza watoto kwa jitihada zao. Upendezi waonyeshwa katika kazi yao ya shule na wapewa kitia-moyo na msaada katika maeneo ambayo wana matatizo. Mwenyekiti amalizia kwa kukazia uhitaji wa kuwa na masilahi ya mtoto moyoni nyakati zote. Ikiwa habari kutoka Amkeni! la Novemba 8, 1990 haipatikani, basi sehemu hii yaweza kutegemea habari katika kitabu Maisha ya Jamaa peke yacho.
Dak. 20: “Njoni Kwenye ‘Lugha Iliyo Safi’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1990.”—Sehemu ya Kwanza. Mazungumzo Pamoja na wasikilizaji ya mafungu 1-14 na pitio fupi la “Vikumbusho vya Mkusanyiko wa Wilaya.”
Wimbo 43 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Tia ndani shukrani za Sosaiti kwa michango, na upongeze kundi kwa ajili ya kutegemeza kifedha mahitaji ya kundi lenu. Hoji kifupi familia ambayo inapanga kuwa na mwisho-juma kamili wa utendaji wa utumishi wa shambani, ukikazia mipango ambayo yaweza kuwa yenye msaada kwa wengine.
Dak. 20: “Kujenga Mahusiano ya Karibu ya Familia.” Hotuba ikitolewa na mzee, pamoja na ushirika fulani wa wasikilizaji. Tia ndani madokezo kuhusu yale yanayoweza kufanywa kwenu ili kujenga sifa za kiroho katika washiriki wa familia na kusaidia wote waonee shangwe utendaji wa utumishi.
Dak. 15: “Njoni Kwenye ‘Lugha Iliyo Safi’ Mkusanyiko wa Wilaya wa 1990.”—Sehemu ya Pili. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji ya mafungu 15-28 ya nyongeza. Kazia kanuni za Kimaandiko zinazopaswa kuongoza mwenendo wetu kwenye mkusanyiko. Watie moyo akina ndugu wapitie nyongeza hiyo pamoja na wanafunzi wa Biblia na kuwasaidia wapange kuhudhuria.
Wimbo 42 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Sanduku la Swali. Toa ripoti juu ya maendeleo ya kampeni ya uandikishaji wa Amkeni!
Dak. 15: Kuthamini Kazi ya Mwangalizi wa Mzunguko. Zungumza pamoja na wasikilizaji habari chini ya “Mwangalizi wa Mzunguko” katika kurasa 47-50 za kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu. Mwenyekiti apaswa akazie jinsi sisi tunavyoweza kunufaika kwa kuunga mkono kikamili ziara. Twapaswa tuthamini kielelezo cha ujitoaji kimungu kinachowekwa na mwangalizi wa mzunguko na mke wake katika kutekeleza migawo yao.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kuzungumza na Watu.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya habari. Uwe na maonyesho mawili yaliyotayarishwa vizuri kuonyesha jinsi ya kuanza mazungumzo mlangoni na tunapokuta watu nje.
Wimbo 20 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA OKTOBA 29
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote watoe ushahidi wa magazeti siku ya Jumamosi.
Dak. 15: Kuwathamini Watumishi wa Huduma Wetu. Hoji akina ndugu wanaoshughulikia jukwaa na vikuza sauti, hesabu, fasihi, magazeti, na wajibu mbalimbali wakiwa wakaribishaji. Toa muhtasari wa wajibu wao hususa na jinsi wahubiri wanavyoweza kushirikiana nao kufanya kazi yao iwe yenye kuonewa shangwe zaidi. Patanisha na mahitaji ya kwenu.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu. Au, “Kuwahi na Wewe.” Hotuba ikitolewa na mzee mwenye mipango mizuri ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1990, kurasa 26-29.
Dak. 15: Tayarisha kwa Ajili ya Huduma ya Novemba. Zungumza mambo ya kuzungumziwa ambayo yangefaa kutumiwa katika eneo lenu katika kutoa New World Translation of the Holy Scriptures na “ Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” au Should You Believe in the Trinity? Toa wonyesho wa jinsi mhubiri aweza kunena na mwenye nyumba juu ya umaana wa kusoma Biblia. Aweza kutumia 2 Timotheo 3:16, 17 kuonyesha kwamba Neno la Mungu limevuviwa na ni lenye manufaa, halafu atumie Yohana 17:3 kuonyesha manufaa hususa. Unganisha na toleo la Novemba.
Wimbo 8 na sala ya kumalizia.