Vijana—Elekezeni Hatua Zenu kwa Ustadi
1 Baba yetu, Yehova, hupendezwa kibinafsi na maendeleo ya kiroho ya vijana. Kwa kusikiliza amri zake za upendo kwa hekima, vijana hufurahisha si moyo wa Yehova tu bali pia hupata burudisho kwa nafsi zao. (Mit. 27:11; Mt. 11:28-30) Wanamruhusu Yehova aandae mwelekezo stadi kwa hatua zao.—Mit. 16:9.
2 Kristo Yesu aliweka mfano katika ujana wake akiwa yule ambaye alipata kibali cha Mungu na wanadamu. (Lk. 2:52) Vijana wanapaswa kufanya vivyo hivyo leo. Mwelekezo stadi wa hatua za kijana wapaswa kuwa dhahiri katika kufuatia kwake mambo ya kiroho. Akiwa na umri wa miaka 12, Yesu alijulikana kwa tamaa yake ya kuongea na wengine juu ya Yehova. (Lk. 2:46, 47) Leo vijana wameonyesha tamaa kama hiyo ya kuelezea wengine juu ya imani yao.—w90-SW 7/1 kur. 29-30; w87-SW 12/1 uku. 21.
3 Ninyi vijana mwaweza kufanya nini sasa hasa wakati wa miezi ya likizo ili ‘kumheshimu BWANA [Yehova, NW] kwa mali yenu’? (Mit. 3:9) Kwa nini usiongeze wakati ambao wewe hutumia katika kazi ya kuhubiri na kufundisha habari njema, hata labda kuwa painia msaidizi? Unaweza kushangazwa na shangwe yenye kuongezeka na manufaa nyingine zinazotokana na ushiriki wenye kuongezeka wa huduma. Hilo pia litakupa fursa ya kufanya kazi shambani na hesabu kubwa ya wahubiri mbalimbali. Unaweza kuanza sasa kwa kumkaribisha mhubiri mmoja au wawili wenye ujuzi ili kufanya kazi nawe mwisho juma huu.
4 Wazazi wanaweza kuwapa watoto wao kitia-moyo kikubwa na msaada kupitia kipindi cha mazoezi pamoja na kuandamana nao kwenye huduma. Wengine waliokomaa katika kundi wanaweza kuchukua hatua ya kwanza kuwauliza vijana waandamane nao kwenye huduma ya mlango kwa mlango na katika kazi ya ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia. Ushirikiano wa karibu na wahubiri hao waliokomaa kiroho utaimarisha vijana na kuwasaidia ‘kukaza mwendo kufikilia utimilifu [ukomavu].’—Ebr. 6:1.
5 Kila Mkristo ana uhitaji wa kuongeza uwezo wake wa kufundisha. Vijana vilevile wanatiwa ndani. Je! ninyi vijana mnatayarisha vizuri migawo ambayo huenda mkapendelewa kutoa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? Je! mna ratiba ya kawaida ya kusoma na kujifunza kibinafsi na kutafakari pia? Je! mnatumia binafsi mambo mnayojifunza? Je! mnatayarisha vizuri mikutano ili kwamba muelewe kikamili na mwe tayari kutoa maelezo? Je! wewe huandika mambo makuu yanayotolewa wakati wa mikutano na kujaribu kutumia madokezo yanayotolewa katika Huduma ya Ufalme Yetu?
6 Usiache fursa za kushiriki kusafisha Jumba la Ufalme na kuwasaidia wazee-wazee au ndugu na dada walio dhaifu kimwili na kazi au kwa njia nyinginezo zenye mafaa. Usiache kutoa michango yako mwenyewe ya kawaida ya kusaidia kutunza gharama za Jumba la Ufalme na kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote.
7 Ikiwa ‘tutalifuata neno la Yehova’ na tumruhusu aelekeze hatua zetu, atatuongoza kwenye furaha na mapendeleo ya utumishi yenye kuongezeka.—Zab. 119:9.