Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/94 uku. 3
  • Ufundishaji wa Kimungu Watoa Uchocheo Wenye Nguvu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufundishaji wa Kimungu Watoa Uchocheo Wenye Nguvu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Furahia Manufaa za Ufundishaji wa Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Ufundishaji wa Kimungu Hushinda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Kufundishwa na Yehova Hadi Siku Hii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Mikusanyiko Yenye Kusisimua Yaendeleza Ufundishaji wa Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 1/94 uku. 3

Ufundishaji wa Kimungu Watoa Uchocheo Wenye Nguvu

1 Tumependelewa kama nini kupokea mafundisho kutoka Yule Mungu, Muumba wetu, Yehova Mungu! (Zab. 50:1; Isa. 30:20b) Kutoka kwa mataifa yote leo, umati unamiminika katika mlima wake wa ibada safi ili kufundishwa naye. (Mik. 4:2) Mamilioni ya wengine hujiandikisha katika shule zinazotukuza kufikiri kwa kibinadamu na hekima ya kilimwengu. Lakini hekima inayopuuza Yehova na Neno lake lililoandikwa ni pumbavu mbele ya Mungu, na wale wanaoongozwa nayo huwa wapumbavu.—Zab. 14:1; 1 Kor. 1:25.

2 Hivi karibuni katika mkusanyiko wetu wa wilaya, tuliona kwa njia isiyo na kifani uwezo wa ufundishaji wa kimungu. Kichwa cha “Ufundishaji wa Kimungu” kilienea programu yote. Tulijifunza kwamba Neno la Mungu pamoja na roho yake hutuunganisha katika udugu wa ulimwenguni pote, ukirekebisha nyutu zetu hutulinda na mafundisho ya mashetani, na kutuzoeza kuwa wahudumu wema. Je! wewe binafsi umenufaikaje na ufundishaji wa kimungu?

3 Matokeo Katika Maisha ya Kikristo: Ufundishaji wa kimungu husaidia kurekebisha dhamiri zetu. Kila mtu amezaliwa akiwa na dhamiri, lakini ili ituongoze kwenye njia ya uadilifu na katika utumishi unaompendeza Yehova, ni lazima izoezwe. (Zab. 19:7, 8; Rum. 2:15) Watu wa ulimwengu hawajarekebisha kufikiri kwao kulingana na Neno la Mungu, na kwa sababu hiyo wamevurugika na hawana uhakika juu ya ni nini lililo sawa na lililo baya. Mabishano hutokea juu ya adili na masuala ya kiadili kwa sababu kila mmoja akazia kufanya yaliyo sawa machoni pake. Walio wengi wataka uhuru wote ili waamue mwendo wao wenyewe wa maisha. Wanakataa kutii chanzo pekee cha hekima ya kweli. (Zab. 111:10; Yer. 8:9; Dan. 2:21) Lakini ufundishaji wa kimungu umetushauri juu ya masuala hayo, na twabaki tumeunganika tukiwa watu wa nyumba ya Mungu kwa sababu twafundishwa naye. Twakabili wakati ujao kwa uhakika tukiwa na dhamiri njema, tukiwa wenye shughuli katika huduma yetu.

4 Ufundishaji wa kimungu hutusaidia tukinze “kila upepo wa elimu.” (Efe. 4:14) Hatujazwi na elimu ya filosofia, ambayo hufanya watu wawe wenye kutafuta makosa na wachunguzi zaidi, wenye kutia moyo maazimio ya mtu mwenyewe, na yanayoongoza kwenye mshuko wa maadili. Twafurahia kufundishwa na Yehova, na hivyo kuepuka huzuni na maumivu ya moyo yanayowapata wengi. Sheria na vikumbusha vya Yehova ni kama ‘neno nyuma yetu,’ linalosema: “Njia ni hii, ifuateni.”—Isa. 30:21.

5 Mikutano Yetu na Huduma Yetu: Sisi twaona Waebrania 10:23-25 kuwa amri kutoka kwa Mungu. Katika mikutano ya kutaniko, twafundishwa na Yehova. Je! ni desturi yetu sikuzote kuwepo mikutanoni, au sisi huona uhudhuriaji wa mikutano kuwa jambo lisilo la maana sana? Kumbuka, kukutana pamoja ni sehemu ya ibada yetu. Haipaswi kuonwa kuwa isiyo ya lazima. Hatupaswi kukosa sehemu yoyote ya ulishaji wa kiroho ambao Yehova ameandaa kwa ajili yetu.

6 Musa alisali kwa Mungu: “Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, tujipatie moyo wa hekima.” (Zab. 90:12) Je! hii pia ni sala yetu? Je! sisi huthamini kila siku yenye thamani? Ikiwa ndivyo, ‘basi tutajipatia moyo wa hekima’ kwa kutumia kila siku katika njia yenye kustahiki, kwa utukufu wa Mfunzi wetu Mtukufu, Yehova Mungu. Ufundishaji wa kimungu utatusaidia kufanya hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki