Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/94 uku. 3
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Uwe Mwangalifu Unapokuwa Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • ‘Toa Ushahidi Kamili’—Kwa Kuhubiri Katika Nyumba za Ghorofa Zenye Wapangaji
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kutangaza Habari Njema-Kwa Kutoa Ushahidi kwa Ujasiri Katika Eneo la Biashara
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 11/94 uku. 3

Sanduku La Swali

◼ Ni tahadhari gani inayohitajiwa tunapohubiri maeneo hatari?

1 Kwa kuongezeka, twasikia ripoti za jeuri, uvunjaji, na vurugu ya kijamii, hasa katika maeneo ya mijini. Ingawa twahisi tukiwa na hangaiko, twajua kwamba hata katika maeneo yasiyo na utulivu kuna watu wenye moyo mnyoofu, watakaoitikia ujumbe wa Ufalme. Kwa hiyo kwa wakati unaofaa, twapaswa kuwa na ujasiri wa kusonga mbele, tukiwa na uhakika na utunzi wa Yehova.—Mit. 29:25; 1 The. 2:2.

2 Tunapoenda kwenye eneo linalokadiriwa kuwa na hatari, Yehova hututazamia tuwe wenye kutahadhari na tutumie uamuzi mzuri. Uwe chonjo. “Mwenye busara huyaona mabaya na kujificha; bali wajinga huendelea mbele wakaumia.” (Mit. 22:3) Wahubiri wenye ustadi wanathamini hekima ya kuhubiri pamoja na wengine wakiwa wawili wawili au katika vikundi vya wahubiri kadhaa, ikiwa ni lazima. Mhubiri 4:9, 12 husema: “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja . . . Hata ikiwa mtu aweza kushinda yule aliye peke yake, wawili watampinga.” Wahalifu hutafuta wale walio peke yao na hivyo rahisi kushambulia.

3 Usibishane na wale wanaoweza kuonekana kuwa wenye kutisha au kushindana. Uwe mwepesi kujitambulisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Wahubiri fulani hubeba Biblia au gazeti Mnara wa Mlinzi au Amkeni! mikononi mwao kwa kusudi la utambulisho.

4 Watupie jicho watu mmoja-mmoja wanaozurura kwenye eneo hilo. Tahadhari unapoingia lifti pamoja na watu wasioonekana kuwa wenyeji wa jengo hilo. Usivae vito vya thamani vyenye bei mno. Ikiwa ni lazima uwe nje baada ya giza kuingia, epuka kutembea kwenye barabara zilizo na giza ambapo kuna magari ya usafiri machache. Ikiwa umepatwa na wanyang’anyi, usikinze ikiwa tu ni pesa au mali zako wanazotaka; uhai wako ni wenye thamani zaidi ya kitu chochote cha kimwili ulicho nacho.—Mk. 8:36.

5 Ndugu wanaoongoza wanahitaji kuwa chonjo, wakijua pale wahubiri wapo katika eneo. Kwa kawaida ni vizuri kufanya kikundi kishughulike sana na eneo hilohilo ili wengine wawe karibu sikuzote. Jeuri ya aina yoyote au msukosuko ukitokea katika ujirani, kikundi chapaswa kuondoka eneo hilo mara moja.

6 Tukiwa chonjo na wenye tahadhari, twaweza kuendelea kuwafikia wale walio kwenye maeneo yenye jeuri sana “wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika.”—Eze. 9:4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki