Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/12 uku. 1
  • Uwe Mwangalifu Unapokuwa Katika Huduma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mwangalifu Unapokuwa Katika Huduma
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Uwe Mwenye Matokeo Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 5/12 uku. 1

Uwe Mwangalifu Unapokuwa Katika Huduma

1. Kwa nini ni lazima tuwe wenye tahadhari tunapohubiri?

1 “Kama kondoo katikati ya mbwa-mwitu,” watumishi wa Mungu wanahubiri “katikati ya kizazi kilicho kombo na kilichopotoka.” (Mt. 10:16; Flp. 2:15) Kila mahali kuna ripoti zenye kutia hofu za misukosuko ya kijamii, vitendo vya jeuri vinavyofanywa na vikundi vya watu wenye fujo, na utekaji nyara unaotekelezwa na watu wakatili. Ripoti hizo zinathibitisha kwamba watu waovu wanaendelea “kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi.” (2 Tim. 3:13) Ni kanuni gani za Kimaandiko tunazoweza kutumia ambazo zitatusaidia ‘tujionyeshe wenyewe kuwa wenye kujihadhari’ katika huduma?—Mt. 10:16.

2. Ni hali gani zinazoweza kufanya liwe jambo la busara kuondoka kwenye eneo na kwenda kuhubiri sehemu nyingine?

2 Tenda kwa Werevu: Andiko la Methali 22:3 linakazia hekima ya ‘kujificha’ ili tusipatwe na msiba. Kaa chonjo! Hali zinaweza kubadilika bila kutazamia katika maeneo ambayo kwa kawaida huwa salama. Unaweza kuona pilikapilika za askari zikiongezeka au makundi ya watu yakijikusanya mitaani. Nyakati nyingine mwenye nyumba mwenye fadhili atakutahadharisha. Badala ya kusitasita ili kudadisi-dadisi, ni jambo la hekima kuondoka mara moja na kuendelea na huduma mahali pengine.—Met. 17:14; Yoh. 8:59; 1 The. 4:11.

3. Kanuni iliyo kwenye Mhubiri 4:9 inaweza kutumikaje katika huduma yetu?

3 Hubiri Pamoja na Wengine: Andiko la Mhubiri 4:9 linasema hivi, “Wawili ni afadhali kuliko mmoja.” Huenda umezoea kufanya utumishi ukiwa peke yako bila kukabili hatari, lakini je, sasa ni salama kufanya hivyo? Katika maeneo fulani kuna usalama. Lakini katika maeneo mengine, siku hizi ni hatari kwa dada au kijana kuhubiri nyumba kwa nyumba akiwa peke yake, na hasa baada ya jua kutua. Mambo ambayo yametukia yanaonyesha wazi kwamba kuwa na mwandamani aliye makini ni jambo muhimu sana. (Mhu. 4:10, 12) Mnapohubiri mkiwa kikundi, kila mmoja anapaswa kuangalia ikiwa washiriki wengine katika kikundi wako salama. Uwe na mazoea ya kuwajulisha wengine unapoondoka kwenye eneo.

4. Tunaweza kufanya nini ili kuchangia usalama wa washiriki wote wa kutaniko?

4 Kama wale ‘wanaoendelea kuzilinda nafsi zetu,’ wazee wana wajibu wa kutoa mwongozo unaofaa kulingana na hali za eneo. (Ebr. 13:17) Kwa hakika Yehova atatubariki tunapokuwa wenye kiasi na kushirikiana nao kwa ukamili. (Mika 6:8; 1 Kor. 10:12) Watumishi wote wa Mungu na watoe ushahidi mzuri, huku wakiwa waangalifu siku zote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki