Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/95 uku. 3
  • Uwe Mwenye Kujenga

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mwenye Kujenga
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Mazungumzo ya Kiroho Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Uwe Mwenye Kujenga na Kutia Moyo
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kujengana Tunapokuwa Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Tunaweza Kutiaje Wema-adili Katika Imani Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 7/95 uku. 3

Uwe Mwenye Kujenga

1 Kwa kuwa twaishi katika ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo,’ sisi sote twahitaji kitia-moyo. (2 Tim. 3:1, NW) Akitambua sana uhitaji huu hata katika siku yake, Paulo alitamani kutumia ushirika akiwa na ndugu zake kama fursa za ‘badilishano la kitia-moyo.’ Aliwasihi ndugu zake ‘wafuate mambo . . . ya kujengana.’ (Rum. 1:11, 12, NW; 14:19) Jitihada hizo zilifanikiwa kwa ‘kufanya imara roho [“nafsi,” NW] za wanafunzi na kuwaonya wakae katika imani.’ (Mdo. 14:22) Twahitaji sana aina hiyo ya kitia-moyo leo.

2 Twaweza kujenga wengine kwa yale tunayosema. Maneno yetu yakitumiwa vizuri, yanaweza kuwa “kama machungwa katika vyano vya fedha.” (Mit. 25:11) Kwa kushiriki katika mikutano, ‘tunatiana moyo.’ (Ebr. 10:25, NW) Ulimi wetu waweza kutumiwa kwa njia chanya tunaposhiriki mambo yaliyoonwa, kutoa pongezi, au kuzungumzia mambo ya kiroho. Utumizi huo wenye kufaa wa ulimi ni ‘mwema wa kumfaa mwenye kuhitaji, ili uwape neema wanaousikia.’—Efe. 4:29.

3 Zungumza Kuhusu Mambo Yajengayo: Kwenye Wafilipi 4:8, Paulo aliandaa miongozo isaidiayo kwa usemi wetu. Alisema twapaswa kufikiria mambo yoyote yaliyo ya kweli, ya hangaikio zito, ya uadilifu, safi, yenye kupendeka, yanayosemwa vizuri, yenye wema-adili, na yenye kustahili sifa. Sikuzote twaweza kuwa na uhakika kwamba yale tusemayo yatakuwa ya kweli na yenye kunufaisha wengine ikiwa yanategemea Neno la Mungu. (Yn. 17:17) Wakfu wetu wa Kikristo, yale tunayojifunza kwenye mikutano ya kutaniko, njia tunayotimiza huduma yetu kikamili, na mambo mengine kama hayo ni mambo ya hangaikio zito. Mazungumzo yenye kujenga kuhusu viwango na kanuni za Neno la Mungu kwa hakika yatatusaidia ‘kutuhekimisha hata tupate wokovu.’ (2 Tim. 3:15) Twaweza kuonyesha uthamini wetu kwa mwenendo safi unaoonyeshwa na wale walio katika tengenezo safi la Yehova. Twaweza kusifu matendo ya fadhili yenye kupendeza ya ndugu zetu. (Yn. 13:34, 35) Mambo yenye kusemwa vizuri hutia ndani sifa zifaazo za Kikristo za imani, shangwe, amani, na uvumilivu tunazoona kwa ndugu zetu. Mazungumzo juu ya mambo kama hayo yenye wema-adili na yenye kustahili sifa ni ‘mema yenye kujenga’ wengine.—Rum. 15:2.

4 Kila siku, twakabiliwa na mahangaiko yenye kuvunja moyo ya huu ulimwengu. Lo! jinsi inavyoburudisha kutoyafikiria na kushiriki ushirika wenye upendo pamoja na ndugu zetu! Wakati wenye thamani tunaoweza kutumia pamoja ni hazina ya kuthaminiwa. Ikiwa sikuzote tu wenye kutia moyo na kujenga, wengine kwa kweli watasema hivi juu yetu: “Wameniburudisha roho yangu.”—1 Kor. 16:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki