“Hubirini Eneo Lenu Kikamili”
1 Kwenye maeneo yanayokaliwa na watu mara kwa mara sisi hukuta sehemu ya biashara ndogondogo, kama duka, kioski, au mkahawa. Ikiwa zote hizo zapasa kuhubiriwa pamoja na sehemu ile nyingine ya eneo hilo, mwapaswa kuzitembelea sawa na zile sehemu za kukaliwa na watu.
2 Mwaweza kutumia utoaji sahili ulio mfupi, labda kwa kusema hivi: “Nina kitu fulani ambacho ningependa kukuonyesha.” Ikiwa mwenyeji aonekana kuwa na shughuli nyingi wakati huo, waweza tu kutoa trakti na kusema hivi: “Nitakuja tena wakati ambapo hutakuwa na shughuli nyingi hivi. Ningependa kujua maoni yako juu ya trakti hii.”
3 Hakuna haja ya kuhofu kufanya kazi hii. Mtangazaji mmoja aliripoti hivi: “Nilitarajia kwamba itikio lisingekuwa zuri. Hata hivyo, kwa mshangao wangu, itikio kwa ujumbe wa Ufalme lilikuwa tofauti kabisa. Walikuwa wenye adabu na wenye urafiki kikweli na walikubali magazeti karibu sikuzote.”
4 Mwanamke anayefanya kazi katika kampuni ya kuuza nyumba na mashamba aliwakaribisha Mashahidi ofisini mwake. Alikubali magazeti na kueleza kwamba angependa kuwa na funzo la Biblia. Alionyeshwa kitabu Ujuzi, na funzo likaanzishwa papo hapo, ofisini mwake!
5 Mgawo wa kuhubiri eneo lenu kikamili hutia ndani kuwatembelea watu ambao wana biashara katika ujirani. (Mdo. 10:42) Panga kuwatembelea kama tu nyumba za faragha. Zaidi ya kulihubiri eneo lenu kwa ukamili zaidi hilo laweza pia kuwathawabisha kwa kuwapa mambo yaliyoonwa yenye kufurahisha!