Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
“Kuiweka Karibu Akilini Siku ya Yehova” ndicho kitakachokuwa kichwa cha programu ya kusanyiko la mzunguko la siku mbili kuanzia Septemba. (2 Pet. 3:12) Imekusudiwa kuamsha hisi yetu ya uharaka. Hivi karibuni wakazi wa dunia wataona hukumu za Yehova. Ni nani atakayeokoka “siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote?” Ni wale tu wanaodumu kuwa macho kiroho na wanaothibitisha kiolezo cha maisha cha “matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu.”—Ufu. 16:14; 2 Pet. 3:11.
Ubatizo ni muhimu kwa mtu ili aokoke siku ya Yehova. (1 Pet. 3:21) Wahubiri wanaotamani kubatizwa kwenye kusanyiko wanapaswa kumwambia mwangalizi-msimamizi, atakayefanya mipango ihitajikayo.
Mfululizo wenye sehemu nne, “Namna ya Watu Tunaopaswa Kuwa,” utaonyesha waziwazi matendo yanayohusishwa katika kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova. Hotuba ya watu wote, “Tenda kwa Hekima Siku ya Yehova Ikaribiapo,” itaeleza linalomaanishwa na ‘kumtafuta Yehova, uadilifu, na usikivu,’ ili kuwa mwokokaji.—Sef. 2:3, NW.
Kusanyiko la mzunguko litamalizia kwa hotuba mbili zenye kuchochea zitakazotolewa na waangalizi wasafirio, zenye vichwa: “Maisha Yako Yanakazia Kweli?” na “Kupangia Kimbele Siku ya Yehova Ikiwa Akilini.” Hotuba hizi zitatuchochea tuchunguze maisha yetu na kufanya marekebisho yanayohitajiwa. Unabii wa Biblia na matukio ya ulimwengu huonyesha waziwazi kwamba siku ya Yehova iko karibu. Programu hii ya kusanyiko itatutia moyo ‘tutunze akili zetu na kuwa wenye kulinda.’ (1 Pet. 5:8) Fanya mipango hususa ya kuhudhuria siku zote mbili.