Jinsi Ambavyo Washiriki wa Familia Hushirikiana ili Kushiriki Kikamili—Katika Huduma
1 Ni nini ambacho kingeweza kuchangamsha moyo zaidi ya kuona waume na wake, wazazi na watoto wakihubiri pamoja katika huduma ya Kikristo, wakilisifu jina la Yehova hadharani? (Zab. 148:12, 13) Familia zote zapasa kuwa na ratiba nzuri ya kawaida ya kushiriki katika utumishi wa shambani. Je, familia yako imetenga siku kila juma ya kushiriki katika huduma? Ikiwa ndivyo, basi kila mtu ajua hasa jambo la kupanga na anaweza kushiriki kikamili.—Mit. 21:5a.
2 Mbona msifanye uwe mradi kutayarisha mapema kabla ya siku ya familia ya utumishi, utoaji mbalimbali ambao familia yenu itatumia? Kujizoeza kwaweza kusaidia zaidi, na kwaweza kutokeza roho ya ushirikiano wa kweli ya familia. Inathawabisha kama nini huduma ya shambani inapokuwa jambo muhimu la familia na washiriki wote wanapojitayarisha vizuri!
3 Mwangalizi asafiriye alijiunga na familia nzima katika utendaji wa magazeti. Alipokuwa akihubiri nyumba hadi nyumba na mmoja wa mabinti wa familia hiyo, binti huyo alimwuliza: “Utahubiri nami kwa muda gani?” Kisha binti huyo akamweleza kwamba angeenda kuhubiri na baba yake baada ya hapo. Ilikuwa dhahiri kwamba yeye na baba yake walifurahia kuwa katika utumishi pamoja. Hiyo ni roho nzuri ya familia kama nini!
4 Huenda familia nyingine zikaweza kufanya upainia-msaidizi kwa mwezi mmoja mwakani. Au huenda ikawezekana angalau mshiriki mmoja wa familia kutumikia akiwa painia-msaidizi wa mfululizo au hata kujiandikisha kuwa painia wa kawaida. Kukiwa na mpango mzuri na ushirikiano, labda washiriki wote wa familia wangeweza kuongeza utumishi wao binafsi kwa kuunga mkono yule anayepainia. Bila shaka familia itabarikiwa kwa utendaji huu ulioongezeka na kwa mambo mazuri yaliyoonwa yanayofurahiwa katika huduma.—Mal. 3:10.
5 Kushiriki kikamili katika kazi ya kueneza evanjeli kutasaidia familia ziwe na uhusiano wa karibu, ziwe na bidii, ziwe na matokeo, na ziwe na furaha katika utumishi wa Yehova!—Linganisha Wafilipi 2:1, 2.