Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/00 uku. 1
  • “Lihubiri Neno . . . kwa Hima”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Lihubiri Neno . . . kwa Hima”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Hisi Yako ya Uharaka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Wanahitajiwa kwa Haraka—Wafanya Kazi Zaidi wa Mavuno!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Kuzidi Kutoa Ushahidi Mwisho Ukaribiapo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 2/00 uku. 1

“Lihubiri Neno . . . kwa Hima”

1 Ukipokea kitu fulani kilichoandikwa “Hima,” maoni yako huwa nini kukihusu? Neno “hima” humaanisha “uhitaji wa kukazia fikira bila kukawia.” Kwa sababu nzuri, mtume Paulo aliagiza Wakristo ‘walihubiri neno . . . kwa hima.’ (2 Tim. 4:2) Je, waitikia kwa kukazia fikira kazi hii bila kukawia?

2 Huenda ikawa iliripotiwa kwa Paulo kwamba baadhi ya ndugu zake walikuwa wakionyesha mwelekeo wa ‘kucheza-cheza katika shughuli yao’ wakiwa Wakristo. (Rom. 12:11) Hilo lilipunguza matokeo ya kazi yao na vilevile shangwe ambayo wangepata kwa kuwasaidia wengine.

3 Maoni ya Yesu Kuhusu Huduma: Yesu alifurahi kama nini kutekeleza huduma yake! Yeye alisema hivi: “Chakula changu ni kwamba mimi nifanye mapenzi yake aliyenituma na kumaliza kazi yake.” Kielelezo cha Yesu kilichochea wanafunzi wake, ambao aliwatia moyo kwa kuwaambia kwamba ‘mashamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.’ (Yn. 4:34, 35) Hisi ya uharaka aliyoonyesha katika huduma yake yote ilikuwa dhahiri alipowaambia wanafunzi wake ‘wamwombe Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.’ (Mt. 9:38) Yesu alifahamu kwamba utume wake ulikuwa kuhubiri, naye alikuwa ameazimia kutoacha kitu chochote kimzuie kufanya hivyo.

4 Vipi Sisi? Leo, kuna uharaka mkubwa zaidi wa kusonga mbele na kazi ya kuhubiri kuliko wakati mwingine wowote. Katika sehemu nyingi za ulimwengu, mashamba ni meupe kwa ajili ya mavuno. Hata katika nchi ambazo zaonekana kama kwamba ushahidi umetolewa, maelfu wanabatizwa kila mwaka. Mwisho wa mfumo huu wa mambo ukaribiapo kwa uharaka sana, kuna “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.” (1 Kor. 15:58) Zaidi ya wakati mwingine wowote, ni muhimu kujikakamua wenyewe kuwaambia wengine ujumbe wa Ufalme.

5 Na tuhangaikie kufikia wengine tukiwa na habari njema, nyumba hadi nyumba na popote pale ambapo watu wanaweza kupatikana katika eneo. Kwa kushiriki kikamili iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri, twaonyesha waziwazi kwamba tumeutanguliza Ufalme maishani mwetu. (Mt. 6:33) Uaminifu wetu katika kuhubiri neno kwa hima utatuletea shangwe nyingi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki