Sanduku la Swali
◼ Ni nani anayepaswa kupata beji ya mkusanyiko wa wilaya?
Beji za mkusanyiko zaweza kusaidia sana kutambulisha ndugu zetu na kutangaza mkusanyiko. Hata hivyo, hazipaswi kugawanywa bila mpango. Hizo humtambulisha mvaaji kuwa mwenye msimamo mzuri akishirikiana na kutaniko hususa la Mashahidi wa Yehova.
Beji hiyo ina mahali pa kuandika jina la mtu huyo na pia kutaniko. Kwa hiyo, lazima mtu huyo awe anashirikishwa kwa kiasi fulani na kutaniko hilo. Sosaiti hutuma beji nyingi kwa kila kutaniko. Ingefaa kumpa beji kila mhubiri aliyebatizwa na asiyebatizwa. Pia, watoto na watu wengine ambao huhudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida na wanaofanya maendeleo kuelekea kushiriki huduma ya shambani wanaweza kupokea moja. Haingefaa kumpa mtu aliyetengwa na ushirika beji ya mkusanyiko.
Beji zipatikanapo, wazee wapaswa kuhakikisha kwamba zinagawanywa kupatana na miongozo hii.