Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/00 uku. 3
  • Je, Wewe Huthamini Mambo Matakatifu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wewe Huthamini Mambo Matakatifu?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1990
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Panga Sasa Kuhudhuria “Wapendao Uhuru” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1991
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1992
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 5/00 uku. 3

Je, Wewe Huthamini Mambo Matakatifu?

1 Tunapoulizwa kama tunathamini mambo matakatifu, labda tungejibu mara moja, ndiyo! Ni nini baadhi ya maandalizi matakatifu ya Mungu tunayothamini?

2 Jinsi tunavyothamini sana uhusiano wa kibinafsi tunaoruhusiwa kuwa nao pamoja na Baba yetu wa kimbingu! Yeye hutuhakikishia kwamba ‘tukimkaribia, naye atatukaribia.’ (Yak. 4:8) Pasipo dhabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo, hakuna mtu ambaye angepokea uhai udumuo milele. (Yn. 3:16) Kupitia sala tunazotoa kila siku, twaonyesha shukrani za moyo mweupe na uthamini wetu wenye kina kwa zawadi hii yenye thamani kutoka kwa Mungu.

3 Neno la Mungu lililopuliziwa, Biblia Takatifu, ni takatifu kwetu pia, kama lilivyo tengenezo la Yehova la kidunia. Twaonyesha uthamini ufaao kwa maandalizi hayo yanayotoka kwa Yehova tunapoishi kupatana na kanuni za Biblia, tunapoimarisha vifungo vya upendo wa kidugu, tunapofuata kwa makini utaratibu wa kitheokrasi, na kushirikiana na wale wanaoongoza.—1 Pet. 1:22.

4 Tunapokea chakula cha kiroho kwa wingi kupitia mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Itakuwa hivyo mwaka huu kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Watekelezaji wa Neno la Mungu.” Huko tutapokea maagizo muhimu na kufurahia ushirika mchangamfu tunaohitaji kwa hima. Tunaweza kuonyeshaje uthamini wa kutoka moyoni kwa ajili ya maandalizi hayo matakatifu?

5 Usipuuze Nyumba ya Yehova: Nehemia aliwaonya kwa upole wale waliofanya kazi kwa bidii kujenga kuta za Yerusalemu ‘wasipuuze nyumba ya Mungu wao.’ (Neh. 10:39, NW) Leo, “nyumba” ya Yehova ni mpango wake wa kuabudu. Mikusanyiko yetu ya Wilaya ni sehemu ya mpango huo. Ili tusipuuze mpango huo, ni lazima tuhudhurie na kusikiliza kwa makini, tukimwonyesha Yehova kwamba tunathamini sana maandalizi hayo. (Ebr. 10:24, 25) Ni mipango gani tunayopaswa kufanya sasa ili kuonyesha tunathamini kikamili tukio hili takatifu?

6 Hudhuria Siku Zote Tatu: Kila mmoja wetu apaswa kupanga kuhudhuria siku zote tatu za mkusanyiko. Je, unapanga kuwasili mapema kila siku na kubaki hadi sala ya mwisho Jumapili? Ikiwa ndivyo, utapata baraka nyingi. Huenda isiwe rahisi siku zote kuhudhuria mkusanyiko. Huenda ukahitaji kuchukua msimamo imara ili kurekebisha ratiba yako ya kazi ya kimwili. Huenda hali ya usafiri isiwe rahisi siku zote. Lakini usiruhusu mambo hayo yakuzuie kuhudhuria mkusanyiko.

7 Fikiria Mfano Huu Ulio Bora Kabisa: Wakiwa njiani kuelekea kwenye mkusanyiko wa wilaya mwaka jana, kikundi cha akina ndugu katika nchi fulani ya Afrika iliyokumbwa na msukosuko wa kijamii walikutana na kikundi cha wanajeshi. Akina ndugu hao wakaulizwa: “Nyinyi ni akina nani, na mwaelekea wapi?” Wakajibu: “Sisi ni Mashahidi wa Yehova, na tunaenda kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya.” Mmoja wa askari akasema: “Nyinyi Mashahidi wa Yehova hamwogopi chochote. Nendeni tu, na mtafanya mkusanyiko wenu bila tatizo lolote. Hata hivyo, mjue kwamba mtakutana na askari wengi. Tembeeni katikati ya barabara wakati wote! Mkiona watu wengi wamekusanyika, endeleeni kutembea katikati ya barabara!” Walifanya hivyo na kufika kwenye mkusanyiko wakiwa salama. Ndugu hao walithawabishwa kwa sababu ya kuthamini mambo matakatifu.

8 Kama ndugu zetu katika sehemu nyingine za Afrika, sisi sote twakabili magumu. Lakini, bila shaka, tunaweza kuiga imani yao na kuazimia kuhudhuria vipindi vyote vya mkusanyiko wetu wa wilaya. Ikiwa wahitaji kufanya marekebisho, mtegemee Yehova ili akuongoze, tukijua kwamba atabariki jitihada zetu ili tuhudhurie programu yote.

9 Pata Baraka: Tuna hamu ya Neno la Mungu, tukijua kwamba kupitia hilo tutapata kukua kufikia wokovu. (1 Pet. 2:2) Tukihudhuria mkusanyiko wa wilaya na kusikiliza programu, sisi sote tutasaidiwa kujenga imani yenye nguvu zaidi katika Neno hilo na hivyo tuweze kukinza ifaavyo mashambulizi ya Shetani. Kwa kufanya hivyo, tutamwonyesha Yehova na watazamaji wote kwamba tunathamini kikamili mambo matakatifu na kwamba “sisi si namna irudiyo nyuma . . . bali namna iliyo na imani kuelekea kuhifadhi hai nafsi.”—Ebr. 10:39; 12:16; Mit. 27:11.

10 Tunaweza kutazamia kwa hamu Yehova Mungu atufungulie madirisha ya mbinguni na kutumwagia baraka nyingi za kiroho. (Mal. 3:10) Weka mradi wa kuhudhuria Mkusanyiko wa Wilaya wa “Watekelezaji wa Neno la Mungu” kuanzia mwanzo kabisa wa programu Ijumaa asubuhi hadi sala ya kumalizia na “Ameni!” Jumapili alasiri. Utafurahi kwamba ulifanya hivyo!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki