Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/00 uku. 3
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwasaidia Wasikilizaji Kutumia Biblia
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kuwaelimisha Wasikilizaji
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kuwatazama Wasikilizaji
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutayarisha Hotuba za Watu Wote
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 9/00 uku. 3

Sanduku La Swali

◼ Kwa nini inafaa wasikilizaji wafungue maandiko wanapoalikwa kufanya hivyo na msemaji wakati wa hotuba yake?

Mambo kama vile habari inayozungumziwa na kama hotuba yahusisha mazungumzo ya mstari kwa mstari ya sehemu ya Neno la Mungu yataamua ni maandiko mangapi wasikilizaji wataombwa kufungua.

Ni jambo la maana kukumbuka kwamba sababu moja ya kufungua maandiko ni kuthibitisha kwamba yale yanayosemwa yanatoka katika Biblia. (Mdo. 17:11) Lengo jingine ni kuchunguza uthibitisho wa Kimaandiko unaopatana na yale yanayozungumziwa ili imani ya wote iimarishwe. Kuona yale ambayo kwa kweli Biblia husema andiko kuu linaposomwa kutafanya wasikilizaji wakumbuke habari hiyo. Pamoja na kufungua maandiko, kuandika na kufuatana na mambo yanayosemwa kunanufaisha.

Ijapokuwa huenda muhtasari uliotolewa na Sosaiti ukataja Maandiko mengi zaidi katika kuzungumzia habari fulani, yameandaliwa kwa manufaa ya msemaji, ili kumsaidia katika kutayarisha hotuba yake. Huenda yakatoa habari inayohusiana nayo na kumsaidia aelewe vizuri kanuni za maandiko zinazohusika na kuelewa jinsi ya kuendeleza habari hiyo. Msemaji anaamua ni maandiko gani yaliyo muhimu ili kusitawisha hotuba na kualika wasikilizaji wafuatane naye maandiko hayo yasomwapo na kuelezwa. Maandiko mengine yanayounga mkono habari hiyo yanaweza kutajwa au kuelezwa kifupi tu, lakini katika visa kama hivyo wasikilizaji hawahitaji kuyafungua.

Msemaji anaposoma maandiko yaliyochaguliwa, apaswa kusoma moja kwa moja kutoka katika Biblia na si kutoka katika karatasi iliyochapishwa kwa kompyuta. Msemaji anapoalika wasikilizaji wafuatane naye katika usomaji, anataja waziwazi kitabu cha Biblia, sura, na mstari au mistari. Anapotua ili kuuliza swali au kueleza kifupi sababu gani andiko hilo lisomwe anaruhusu wasikilizaji wapate wakati wa kufungua andiko hilo. Pia kurudia kutaja andiko kutasaidia wasikilizaji walikumbuke. Hata hivyo, ni afadhali usitaje ukurasa, kwa kuwa hutofautiana ikitegemea hasa tafsiri ya Biblia ambayo watu mmoja-mmoja miongoni mwa wasikilizaji wanatumia. Wanapoalikwa kufungua maandiko, wasikilizaji husaidiwa kunufaika kutokana na nguvu ya Neno la Mungu linapoelezwa wakati wa hotuba.—Ebr. 4:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki