Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya Mwaka 2001
1 Kuna sababu tele za Kimaandiko ambazo zapasa kutufanya sote tushiriki kikamili iwezekanavyo katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.—Mit. 15:23; Mt. 28:19, 20; Mdo. 15:32; 1 Tim. 4:12, 13; 2 Tim. 2:2; 1 Pet. 3:15.
2 Programu ya usomaji wa Biblia wa kila juma imekuwa sehemu ya shule kwa muda mrefu. Kwa ujumla inatia ndani kusoma ukurasa mmoja wa Biblia kila siku. Kuanzia mwaka huu, usomaji wa Biblia umeratibiwa pia katika kila juma la pitio la kuandika. Ratiba ya nyongeza ya usomaji ambayo iliratibiwa kwa miaka mitatu iliyopita, imekamilika. Lakini ukitaka kufanya usomaji wa Biblia zaidi ya ule ulioratibiwa, unaweza kutengeneza programu yako mwenyewe ya usomaji.
3 Mgawo Na. 2 huzoeza akina ndugu kwa ajili ya ‘usomaji wa Neno la Mungu mbele ya watu wote.’ (1 Tim. 4:13) Unapokuwa na mgawo wa kusoma, jizoeze kwa sauti ya juu kwa kurudia-rudia. Unaweza kutumia kaseti za Sosaiti za usomaji wa Biblia, ikiwa zapatikana, ili kuboresha matamshi yako, ubadilifu wa sauti, na sehemu nyingine za usomaji mzuri.
4 Mgawo Na. 3 na Na. 4 unategemea kitabu Kutoa Sababu, ambacho kilitayarishwa kwa ajili ya huduma ya shambani. Ikiwa habari uliyogawiwa ni nyingi kuliko unayoweza kutoa kwa wakati uliowekwa, chagua tu habari itakayofaa eneo la kutaniko lenu. Kikao chochote ambacho kitafaa eneo lenu chaweza kutumiwa.
5 Jitahidi uwezavyo kutimiza migawo yako yote katika shule. Tumia wakati kujitayarisha vizuri, na uzungumze kutoka moyoni. Utakuwa chanzo cha kitia-moyo kwa kutaniko, nawe utanufaika kibinafsi kwa kushiriki kwa moyo wote katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi mwaka wa 2001.