Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2002
1 Uwezo wa kusema hauthaminiwi sana na watu wengi. Hata hivyo, uwezo wa kusema ni zawadi kutoka kwa Yehova. Hutuwezesha kuwasiliana na wengine na kueleza mawazo na hisia zetu. Zaidi ya yote, twaweza kutumia uwezo huo kumsifu Mungu.—Zab. 22:22; 1 Kor. 1:4-7.
2 Wanaume, wanawake, na watoto wanazoezwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ili kutangaza jina la Yehova. (Zab. 148:12, 13) Shule ya mwaka wa 2002 itazungumzia mambo mengi sana ambayo sisi binafsi tunaweza kunufaika nayo na kuyatumia katika huduma. Tunaweza kuongeza maarifa yetu na ujuzi wetu wa kufundisha Neno la Mungu tukijitayarisha na kushiriki katika shule.—Zab. 45:1.
3 Soma Biblia Kila Siku: Ikiwa kwa kawaida tunakuwa na Biblia karibu, twaweza kuisoma kila tunapopata nafasi. Wengi wetu huwa na dakika chache za ziada wakati wa mchana ambazo twaweza kuzitumia kufanya hivyo. Utafaidika kama nini kusoma angalau ukurasa mmoja kila siku. Ukifanya hivyo utaweza kwenda sambamba na ratiba ya shule ya usomaji wa Biblia !—Zab. 1:1-3.
4 Uwezo wa kusoma Biblia vizuri unaweza kutusaidia kufikia mioyo ya wasikilizaji wetu na kuwachochea wamsifu Yehova. Akina ndugu walio na Hotuba Na. 2 katika shule wanapaswa kujizoeza, na kujizoeza, na kujizoeza tena, kusoma sehemu aliyogawiwa kwa sauti. Mwangalizi wa shule atawapongeza na kutoa madokezo ya kuboresha usomaji wao.
5 Tumia Kitabu Kutoa Sababu: Hotuba Na. 3 na Na. 4 itatolewa kutoka kitabu Kutoa Sababu. Labda wengi wetu tunaweza kujitahidi mara nyingi kutumia msaada huu katika huduma ya shambani. Akina dada wanapaswa kuchagua vikao ambavyo vyafaana na eneo. Mwangalizi wa shule anapaswa kuzingatia jinsi wanafunzi hao wanavyofundisha na kutumia Maandiko.
6 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na itusaidie sote twendelee kutumia uwezo wa kusema ambao ni zawadi kutoka kwa Mungu ili tutangaze habari njema na kumsifu Mungu wetu mkuu, Yehova!—Zab. 34:1; Efe. 6:19.