Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/01 uku. 6
  • Fanya Mema Usifiwe!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fanya Mema Usifiwe!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • “Dumisheni Mwenendo Wenu Ukiwa Mzuri Katikati ya Mataifa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Mwenendo Unaomtukuza Mungu
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Makusanyiko Yetu ya Wilaya—Ushuhuda Wenye Nguvu wa Ile Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 5/01 uku. 6

Fanya Mema Usifiwe!

1 “Wana utulivu ambao sijapata kuona katika kikundi kingine chochote cha watu.” “Inafurahisha kupata kikundi hiki.” Hayo ni maelezo yenye kujenga yaliyopokewa kutoka kwa watazamaji baada ya mikusanyiko ya wilaya ya mwaka jana, yakionyesha sifa nzuri tuliyo nayo kama tengenezo. (Mit. 27:2; 1 Kor. 4:9) Hatimaye, sifa hiyo humwendea Yehova. (Mt. 5:16) Fursa nyingine nzuri zaidi ya kumsifu Mungu iko mbele yetu mwaka huu kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa “Walimu wa Neno la Mungu.”

2 Kila mwaka sisi hupokea vikumbusha vyenye fadhili kuhusu mwenendo unaofaa kwenye mkusanyiko. Kwa nini? Kwa sababu kadiri mtazamo, mapambo, na tabia ya ulimwengu huu iendeleapo kuharibika, twakataa kuiga tabia hiyo. Hatutaki sifa yetu nzuri iharibike. (Efe. 2:2; 4:17) Na tukumbuke maonyo yafuatayo.

3 Fanya Mema—Hotelini na Kwenye Vyumba vya Kulala vya Shule: Twajulikana kuwa watu wenye kufuata haki. (Ebr. 13:18) Kwa sababu hiyo, twapaswa kusema kweli kuhusu idadi ya watu tunaokaa nao mahali pa kulala. Hatupaswi kupikia kwenye chumba kama hairuhusiwi. Meneja mmoja alisema kwamba alipunguzia Mashahidi wa Yehova bei za chumba kwa kuwa halazimiki kununua tena taulo kwa sababu ya zile nyingine kuibiwa. Anajua kwamba mahali hapo patatunzwa vyema. Kwa kweli hatutachukua “vitu vya kukumbuka” kutoka hotelini. Badala yake, ikiwa ni zoea la hapo, acha bakshishi ya kuonyesha uthamini kwa huduma ulizopewa. Na sikuzote uwe mwungwana na mwenye subira unaposhughulika na wafanyakazi wa hoteli au wakuu wa shule.

4 Watazamaji wanavutiwa wanapoona vijana wetu wakijiendesha kwa upole na kwa utii. (Efe. 6:1, 2) Wazazi, tafadhali simamieni watoto wenu ili wasisumbue wengine, hata wanapokuwa kwenye uwanja wa hoteli au shule. Wote wanapaswa kuepuka kugongesha milango kwa nguvu au kupiga kelele, hasa usiku.

5 Twaweza kufanya mema kwa kuwajali wageni wengine wasio Mashahidi ambao pia wanatumia majengo hayo. Hatupaswi kamwe kuhisi kwamba hatuhitaji kutii miongozo na sheria za hapo.

6 Fanya Mema—Mkusanyikoni: Imeonekana kwamba wakusanyikaji wengine wamekataa kushirikiana na wakaribishaji, hata wameongea nao kwa njia isiyo ya Kikristo. Fuateni maagizo ya akina ndugu na msiegeshe magari mahali pasiporuhusiwa. Hakika, mtazamo wa kujifikiria kwanza haumtambulishi mtu kuwa mtendaji wa mema, wala haumletei Yehova Mungu sifa. Kwa hiyo, acheni tuwe wenye upendo, wenye subira, na wenye kushirikiana.—Gal. 5:22, 23, 25.

7 Tunapotafuta mahali pa kuketi, sisi akina ndugu na dada hatutakimbia na kusukumana ili tupate viti vilivyo “bora.” Twaweza kuumizana kwa sababu ya tabia hiyo. Ijapokuwa imependekezwa tubebe chakula chepesi cha mchana, haifai kuweka meza mahali pa kuegeshea magari ili tuwe na mlo mkubwa.

8 Tufanye Mema—Kwa Mavazi na Mapambo Yetu: Baada ya mmoja wa mikusanyiko ya wilaya ya mwaka jana, mhariri wa kampuni moja kubwa ya magazeti katika jiji moja aliandika hivi: “Zaidi ya kitu kingine chochote, mwenendo wa Mashahidi wenyewe tu ulikuwa wenye kupendeza zaidi. Ilifurahisha kama nini kuona watu wengi sana wakijiendesha kwa njia ya heshima na staha. Wakiwa wamevalia mavazi yao mazuri zaidi, mamia ya familia kutoka jamii na makabila mbalimbali walimiminika kwa utulivu katika uwanja. Tabia yao ilikuwa tofauti sana na ile ya umati wa kawaida unaokwenda uwanjani. Kwa kweli, Mashahidi ni tofauti sana na makundi mengi ya watu kwa ujumla. Limekuwa jambo la kawaida kuona tabia yenye ujeuri mahali pa umma. . . . Kweli, umati wa Mashahidi wafurahisha.” Tusiruhusu kamwe mavazi yetu na mapambo yetu yaharibu kwa vyovyote hali ya kiroho ya mkusanyiko.—Flp. 1:10; 1 Tim. 2:9, 10.

9 Fanya Mema—Wakati wa Ubatizo: Wanaotaka kubatizwa wanapaswa kustahi sana tukio hilo. Kuvalia vazi ambalo linabaki likiwa na kiasi linapoloa kutaonyesha wanathamini utakatifu wa tukio hilo. Itafaa zaidi viongozi wa funzo la Biblia wazungumzie pamoja na wanafunzi wao kabla ya kuhudhuria mkusanyiko “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1995.

10 Mapambo yetu na mwenendo wetu wa kumhofu Mungu washuhudia imani zetu za Kikristo na hufanya iwe rahisi kwa watu wenye unyofu wa moyo kuitambua kweli. Basi, acheni ‘tufulize kufanya lililo jema,’ na tusifiwe tunapohudhuria Mkusanyiko wa Wilaya wa “Walimu wa Neno la Mungu.”—Rom. 13:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki