Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 8
  • Weka Starehe Mahali Panapoifaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Weka Starehe Mahali Panapoifaa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Tafrija Unayochagua Inakujenga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Tafrija Inayoburudisha Kweli Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Tumia Wakati Wako kwa Hekima
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Je, Roho ya Ulimwengu Inakutia Sumu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 8

Weka Starehe Mahali Panapoifaa

1 Katika nyakati hizi zilizo ngumu, sisi sote twahitaji kustarehe mara kwa mara. Kuwa na tafrija kwa kiasi fulani kwafaa. Hata hivyo, mtu anapotumia wakati mwingi sana katika starehe, vitumbuizo, na kutembelea marafiki huenda akatumia wakati mchache sana katika mambo ya kiroho. Lazima tuweke starehe mahali pake panapoifaa. (Mt. 5:3) Hilo lawezekanaje? Kwa kufuata shauri linalopatikana kwenye Waefeso 5:15-17.

2 Weka Mipaka: Paulo aliandika kwamba Wakristo wanapaswa “kuangalia sana” ikiwa wanaishi kwa hekima. Kiasi na kujidhibiti kwahitajiwa ili kuweka mipaka ya starehe zilizo za lazima. Inafaa kufikiria kwa uzito jinsi tunavyotumia nafasi yetu. Tafrija yapasa kutunufaisha badala ya kutufanya tuhisi kwamba tumeharibu wakati wetu au tumechoka. Ikiwa baada ya tafrija tutahisi tumechoka, au tuhisi hatujatimiza chochote, au tuhisi tukiwa na hatia baada ya kufanya shughuli fulani, hiyo itaonyesha kwamba twahitaji kufanya marekebisho ya jinsi tunavyotumia wakati wetu.

3 Kuwa Mwenye Akili: Paulo alitoa shauri la ‘kununua kabisa wakati unaofaa’ kwa ajili ya mambo ya maana zaidi maishani, si kuwa watu wenye “kukosa akili.” Wakristo waliojiweka wakfu hawawezi kuruhusu maisha yao yakazie starehe tu. Ijapokuwa pumziko laweza kutupa nguvu zaidi za kimwili, kani ya utendaji ya Mungu ndiyo hutupa nguvu za kiroho. (Isa. 40:29-31) Twapokea roho yake tunapofanya mambo ya kitheokrasi kama vile, kujifunza Biblia, kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kwenda katika utumishi wa shambani bali si kupitia tafrija.

4 Panga Mambo Unayopaswa Kutanguliza: Paulo aliagiza Wakristo ‘waendelee kufahamu mapenzi ya Yehova ni nini.’ Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kutanguliza mambo yanayohusiana na Ufalme wa Mungu maishani mwetu. (Mt. 6:33) Ni lazima tufanye kwanza mambo yatakayotuwezesha kuishi kulingana na wakfu wetu kwa Yehova. Baadaye, starehe yaweza kuwekwa mahali pake panapoifaa. Tukifanya hivyo, tutapata manufaa ya starehe na kufurahi zaidi.—Mhu. 5:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki