Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 1
  • Tumia Wakati Wako kwa Hekima

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Wakati Wako kwa Hekima
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Weka Starehe Mahali Panapoifaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Jinsi ya Kukomboa Wakati
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Je, Tafrija Unayochagua Inakujenga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wewe Unatanguliza Nini?
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 1

Tumia Wakati Wako kwa Hekima

1 Tamaa yetu ya kumpendeza Yehova hutuchochea kuzingatia mambo ya kiroho maishani. Neno lake linatuagiza ‘tuendelee kutafuta kwanza ufalme’ na ‘kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Mt. 6:33; Flp. 1:10) Tunawezaje kununua wakati kwa ajili ya mambo ya kiroho na kuepuka kutanguliza mambo yasiyo muhimu sana?—Efe. 5:15-17.

2 Tanguliza Mambo ya Ufalme: Panga wakati wako ili usiupoteze katika mambo yasiyo muhimu. Mwanzoni mwa kila mwezi, ndugu fulani hutia alama siku hususa kwenye kalenda yao kwa ajili ya kazi ya kuhubiri. Kisha wanahakikisha kwamba mambo mengine hayavurugi mipango hiyo. Unaweza kufanya vivyo hivyo ili kununua wakati kwa ajili ya mikutano, funzo la kibinafsi, na makusanyiko. Wengi wana ratiba ya kila siku ambayo huanza au kumalizika kwa kusoma Biblia. Tenga wakati hususa kwa ajili ya kila jambo muhimu, na usiruhusu mambo mengine yakuvuruge isivyo lazima.—Mhu. 3:1; 1 Kor. 14:40.

3 Usiutumie Ulimwengu Sana: Katika nchi fulani, kuna fursa nyingi za kujihusisha na mambo kama vile michezo, burudani, tafrija, na shughuli nyingine za kujifurahisha. Wengi hutumia wakati mwingi sana wakitazama televisheni au wakitumia kompyuta. Hata hivyo, hapana shaka kwamba kuzingatia sana vifaa vipya na mambo ya kujifurahisha yanayopatikana katika ulimwengu huu hukatisha tamaa. (1 Yoh. 2:15-17) Kwa hiyo, Biblia inatuhimiza tusiutumie ulimwengu kwa ukamili. (1 Kor. 7:31) Kwa kufuata ushauri huo wa hekima, unaweza kumdhihirishia Yehova kwamba unatanguliza ibada yake maishani mwako.—Mt. 6:19-21.

4 Mwisho wa mfumo huu wa mambo unakaribia. Wale wanaotanguliza mambo ya kiroho watakuwa wenye furaha na watapata kibali cha Mungu. (Met. 8:32-35; Yak. 1:25) Kwa hiyo, na tutumie kwa hekima wakati wetu ambao una thamani kubwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki