Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Kuna watu wapendao kweli katika karibu dini zote. Hata hivyo, inaonekana kwamba dini kwa ujumla huwagawanya wanadamu. Ni jambo gani linalohitajiwa ili kuwaunganisha watu wenye mioyo minyoofu? [Baada ya jibu, soma Sefania 3:9.] Gazeti hili laonyesha jinsi ujuzi kuhusu Mungu wa kweli unavyounganisha watu kila mahali.”
Amkeni! Sept. 22
“Baadhi yetu huona likiwa jambo la kawaida tu kuwa na chakula kingi. Lakini sasa kuna wasiwasi kwamba huenda sayansi inahatarisha chakula chetu. Gazeti hili laeleza baadhi ya mahangaiko hayo na vilevile tumaini la Biblia kuhusu suluhisho halisi kwa tatizo hilo.”
Mnara wa mlinzi Okt. 1
“Huenda ukakubali kwamba si watu wengi wanaopenda kuongea juu ya imani katika Mungu. Lakini kwa nini iko hivyo? [Baada ya jibu, soma Waebrania 11:1.] Gazeti hili laeleza maana ya imani ya kweli na matokeo ya kuwa na imani na kutokuwa na imani.”