Lengo Letu Ni Nini?
1 Kwa nini sisi huongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani? Je, ni kufunza watu ujuzi tu, kuboresha maisha yao, au kufanya wawe na wakati ujao mzuri? La. Lengo letu kuu ni kuwafanya wawe wanafunzi wa Yesu Kristo! (Mt. 28:19; Mdo. 14:21) Ndiyo sababu wale tunaofunza wanahitaji kushirikiana na kutaniko. Maendeleo yao ya kiroho yanahusiana moja kwa moja na uthamini wao kwa tengenezo la Kikristo.
2 Jinsi ya Kufikia Lengo Hilo: Mnapoanza kujifunza, endelea kumsihi mwanafunzi ahudhurie mikutano ya kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Mweleze jinsi mikutano hiyo itakavyoimarisha imani yake, imsaidie kufanya mapenzi ya Mungu na kumwezesha awe na ushirika mzuri pamoja na wengine ambao pia wanapenda kumsifu Yehova. (Zab. 27:13; 32:8; 35:18) Unaposimulia jinsi unavyopenda na kuthamini kutaniko na mikutano, utachochea tamaa yake ya kuhudhuria.
3 Wapya wapaswa kuelewa kwamba tengenezo la Yehova ni udugu wa kimataifa. Ikiwezekana, waonyeshe video Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name na Our Whole Association of Brothers. Wasaidie wafahamu kwamba Yehova anatumia mamilioni ya watu waliojiweka wakfu ulimwenguni pote kutimiza mapenzi yake. Acheni wapya hao wajue kwamba wanaalikwa kumtumikia Mungu pia.—Isa. 2:2, 3.
4 Inafurahisha kama nini kuona mwanafunzi wa Biblia akiwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu. Hilo ndilo lengo letu!—3 Yoh. 4.