Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Des. 15
“Wakati huu, watu wengi wanafikiria juu ya Yesu Kristo, iwe wanamwamini au hawamwamini. Wengine husema kwamba hakuwa mtu halisi. Una maoni gani? [Akijibu, soma Mathayo 16:15, 16.] Nina uhakika kwamba utafurahia kusoma makala hii kuhusu ‘Yule Yesu Halisi’ ili uone jinsi anavyokuathiri leo na jinsi atakavyokuathiri wakati ujao.”
Amkeni! Des. 22
“Je, hukubaliani nami kwamba ili kufanya maisha yawe salama twahitaji chakula cha kutosha kilicho salama? [Ngoja ajibu.] Ona vile Mungu alivyoahidi watu wake nyakati za Biblia. [Soma Mambo ya Walawi 26:4, 5.] Amkeni! huzungumzia wasiwasi tulio nao leo juu ya chakula chetu. Pia gazeti hilo linazungumzia wakati Mungu atakapotupatia usalama ulimwenguni pote.”
Mnara wa Mlinzi Jan. 1
“Je, wewe hujiuliza ni kwa nini watu wengine huwa na maisha mazuri hali wengine hupambana na hali ili kupata riziki? Biblia inatoa jibu. [Soma Ayubu 34:19.] Gazeti hili linazungumzia jinsi ambavyo Mungu anakusudia kukomesha ubaguzi wa kijamii.”
Amkeni! Jan. 8
“Sisi sote tumesikia kuhusu ule msiba uliotikisa ulimwengu. Tangu wakati huo, watu wamehitaji faraja na msaada mwingi. Makala hii yaeleza kile ambacho Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakifanya ili kusaidia waokokaji wa msiba huo, wafanyakazi wa dharura, na wale waliofiwa.”