Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Machi 15
“Je, unakubali kwamba utawala mwadilifu unaweza kufanya dunia iwe mahali bora pa kuishi? [Ngojea jibu.] Tafadhali ona ahadi ya Biblia. [Soma Zaburi 37:11.] Twaweza kufurahia amani hiyo, ambayo itakuwa halisi chini ya Kiongozi anayefaa anayezungumziwa katika makala hizi.”
Amkeni! Machi 22
“Matetemeko ya ardhi yanaweza kusababisha vifo na maangamizi makubwa mno. Mara nyingi waokokaji huachwa bila makao, wakiwa hawana namna ya kurudia hali yao ya zamani. Toleo hili la Amkeni! laonyesha jinsi watu wamekabiliana na hali baada ya tetemeko. Pia laeleza jinsi matetemeko ya ardhi yalivyo sehemu ya maana zaidi ya unabii wa Biblia.”
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Ningependa kuzungumza nawe jambo lenye kutia moyo katika Biblia. [Soma Mathayo 22:37.] Wafikiri hiyo yamaanisha nini? [Ngojea ajibu.] Ona jinsi makala hii inavyosema, ‘Mtafute Mungu kwa Moyo na Akili.’ Je, imani ya kweli yahusisha moyo tu au akili pia? Jibu lake litakufahamisha zaidi.”
Amkeni! Apr. 8
“Kama ujuavyo, kutunza familia ni jambo gumu siku hizi, na kuwa mama ni kazi yenye kudai mengi mno. Toleo hili la Amkeni! lina habari yenye kupendeza yenye kichwa ‘Je, Mama Wana Kazi Nyingi Mno?’ Ningependa kukuachia nakala hii.”