Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mac. 15
“Tungependa kukualika kwa mwadhimisho wa Mlo wa Jioni wa Bwana, Jumapili, Aprili 4. [Eleza ukitumia mwaliko ulio kwenye ukurasa wa nyuma wa gazeti au tumia vikaratasi vya kuwaalika watu kwenye Ukumbusho. Kisha soma Luka 22:19.] Makala za kwanza katika gazeti hili la Mnara wa Mlinzi zinazungumzia tukio hilo na jinsi linavyoadhimishwa.”
Amkeni! Mac. 22
Baada ya kutaja msiba ambao watu wanajua, uliza: “Umewahi kujiuliza ni kwa nini Mungu huruhusu mambo haya yatokee? [Ngoja jibu. Kisha soma Yakobo 1:13.] Makala hii ambayo imeandikwa hasa kwa ajili ya vijana inaeleza ni kwa nini Muumba wetu mwenye upendo hajaingilia mambo na kukomesha kuteseka kwa wanadamu.”
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Si mistari mingi ya Biblia imezua utata sana kama lile andiko linalotaja fumbo la alama ya mnyama-mwitu. Je, umewahi kusikia fumbo hilo? [Ngoja jibu. Kisha soma Ufunuo 13:16-18.] Biblia inatoa vidokezi vya kufumbua fumbo hilo. Gazeti hili linataja vidokezi hivyo.”
Amkeni! Apr. 8
“Watu wengi wanajua simulizi la maisha ya Musa. Lakini je, unajua kwamba Musa alisema jambo fulani ambalo linatuhusu leo? [Ngoja jibu. Kisha soma Kumbukumbu la Torati 18:15.] Gazeti hili la Amkeni! linaeleza nabii anayetajwa katika andiko hilo na jinsi atakavyowanufaisha wanadamu.”