Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/02 uku. 3
  • Badilishano la Kitia-Moyo la Pekee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Badilishano la Kitia-Moyo la Pekee
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Endeleeni Kutiana Moyo Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Je, Wewe Huthamini Mambo Matakatifu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • ‘Wakusanye Watu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 5/02 uku. 3

Badilishano la Kitia-Moyo la Pekee

1 Hakuna siku ambayo hupita bila watumishi wa Yehova kupatwa na majaribu ya imani yao. Ibilisi anajua kuwa ana wakati mchache tu, kwa hiyo anafanya shambulizi la mwisho ili kuvunja uaminifu wetu kwa Yehova. (Ufu. 12:12) Ni muhimu ‘twendelee kujipatia nguvu katika Bwana na katika uwezaji wa nguvu yake’ ili ‘tupate kuweza kukinza katika siku ya uovu na, baada ya [sisi] kuwa tumefanya mambo yote kikamili, kusimama imara.’—Efe. 6:10, 13.

2 Kukusanyika pamoja na waamini wenzetu ni mpango wa Yehova wa kutusaidia tupate nguvu. Mtume Paulo aliuthamini mpango huo. Alitamani kushirikiana na ndugu zake Wakristo ili ‘watiane moyo’ na ‘wafanywe imara.’ (Rom. 1:11, 12) Ili kutuimarisha kufanya mapenzi ya Mungu, kwa upendo Baraza Linaloongoza limepanga kutupa fursa ya kunufaika na badilishano la kitia-moyo kwenye kusanyiko la wilaya linalokuja lenye kichwa “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii.”

3 Fika Ili Ufaidike: Jitahidi kuhudhuria siku zote tatu. Sisi ‘hujinufaisha’ kwa kufika kabla ya wimbo wa kwanza na kungoja hadi tuseme “Amina” wakati wa sala ya mwisho. (Isa. 48:17, 18) Wengi watahitaji kupanga ratiba yao ya kazi mapema sana ili wahudhurie siku zote tatu. Ni kweli kwamba huenda isiwe rahisi kupata ruhusa kutoka kwa mwajiri wako lakini Yehova anatuhakikishia kwamba atatusaidia kufanya mapenzi yake. (1 Yoh. 5:14, 15) Ikiwa bado hatujafanya hivyo, sasa ndio wakati wa kufanya mipango kamili ya usafiri na mahali pa kulala badala ya kungoja hadi dakika ya mwisho. Twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atabariki jitihada zetu za kuhudhuria siku zote tatu.—Mit. 10:22.

4 Tazamia Kitia-Moyo: Je, baada ya kuhudhuria kusanyiko la wilaya umewahi kusema: “Hilo lilikuwa kusanyiko bora zaidi!” Kwa nini ulihisi hivyo? Ni kwa sababu tukiwa wanadamu wasiokamilika twaweza kuchoka polepole, na hivyo kuhitaji kitia-moyo cha kiroho. (Isa. 40:30) Dada mmoja alisema hivi: “Huu mfumo wa mambo hunichosha sana, na makusanyiko hunisaidia kukazia fikira mambo ya kiroho, yakinipa nguvu za kiroho ninazohitaji. Inaonekana kwamba kitia-moyo hicho huja wakati ninapokihitaji zaidi.” Yaelekea umewahi kuwa na hisia kama hizo.

5 Twapokea kitia-moyo kinachohitajika kutoka kwa hotuba na mahojiano na pia kupitia sehemu nyingine zenye kujenga kiroho za makusanyiko yetu. Ndugu mmoja alisema hivi: “Mimi huthamini sana tunapoonyeshwa wazi jinsi ya kutumia kanuni za Biblia. Bila shaka, drama hutusaidia sana kuona jinsi tunavyoweza kujifunza kutokana na mifano mizuri na mibaya ya kale. Sikuzote mimi hungoja kwa hamu vichapo vipya, nami huvifurahia kwa muda mrefu baada ya kurudi nyumbani.”

6 Makusanyiko ni mipango ya maana kutoka kwa Yehova katika hizi “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Tim. 3:1) Makusanyiko hutusaidia tutii shauri hili lililopuliziwa: “Kaeni macho, simameni imara katika imani, endeleeni kama wanaume, kueni mwe wenye uweza.” (1 Kor. 16:13) Kwa hiyo, na tuazimie kuhudhuria vipindi vyote na kufurahia badilishano la kitia-moyo kwenye Kusanyiko letu la Wilaya la “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii”!

[Sanduku katika ukurasa wa 3]

Panga Kuhudhuria Siku Zote Tatu

■ Omba ruhusa kazini.

■ Pangia mapema mahali pa kulala kwenye jiji la kusanyiko.

■ Fanya mipango ya usafiri kwenda kusanyikoni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki