Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/14 kur. 2-3
  • ‘Wakusanye Watu’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Wakusanye Watu’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Sikiliza na Ujifunze
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Pindi ya Kulishwa Kiroho na Kushangilia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Njoni Kwenye “Lugha Iliyo Safi” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1990
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 6/14 kur. 2-3

‘Wakusanye Watu’

1. Makusanyiko ya eneo na ya kimataifa yanalinganaje na kusanyiko kubwa walilofanya Waisraeli muda mfupi baada ya kutoka Misri?

1 Muda mfupi baada ya kutoka Misri, Yehova alimwagiza Musa ‘awakusanye watu’ kwenye Mlima Sinai ili wasikilize neno Lake, wamwogope na wawazoeze watoto wao wafuate njia Zake. (Kum. 4:10-13) Hilo lilikuwa tukio lenye kujenga imani na lisilosahaulika! Katika miezi michache ijayo, watumishi wa Yehova watakusanyika katika makusanyiko ya eneo na ya kimataifa ili wafundishwe na Yehova. Tunapaswa kufanya nini ili tufaidike kikamili?

2. Tunapaswa kufanya nini ili tuwe tayari kwa ajili ya kusanyiko?

2 ‘Muwe Tayari’: Yehova aliwaamuru Waisraeli “wawe tayari” kwa ajili ya kusanyiko hilo kubwa sana kwenye Mlima Sinai. (Kut. 19:10, 11) Vivyo hivyo, wote watakaohudhuria kusanyiko wanahitaji kujitayarisha vizuri, hata kama hawatakuwa na migawo kwenye programu. Kwa mfano, wengi watahitaji kufanya mipango kazini ili waruhusiwe kuhudhuria kusanyiko. Huenda hali yako ikafanana na ya Nehemia. Alitaka kuacha kazi yake akiwa mnyweshaji wa Mfalme Artashasta ili aende Yerusalemu kusaidia kujenga upya kuta za mji huo, lakini alijua kwamba huenda Mfalme asikubali. Nehemia alitoa sala, halafu kwa uhodari akatoa ombi lake kwa maneno ya heshima. Mfalme alimpa ruhusa ya kwenda na hata akategemeza mradi huo wa ujenzi! (Neh. 2:1-9) Zaidi ya kuomba ruhusa kutoka kwa mwajiri wako, je, umehakikisha mipango yako ya usafiri na malazi? Wazee wako tayari kutoa msaada kwa yeyote anayehitaji. Panga kufika mapema programu inapoanza asubuhi na mchana, na uwe tayari ‘kukazia uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida’ mambo utakayosikia.—Ebr. 2:1.

3. Ni nini kitakachotusaidia kutayarisha mioyo yetu kwa ajili ya programu?

3 Ni muhimu pia kutayarisha mioyo yetu ili tuweze kusikiliza na kujifunza. (Ezra 7:10) Programu ya kusanyiko itapatikana kwenye Tovuti ya jw.org/sw kabla ya kusanyiko, na itakuwa na orodha ya vichwa vya hotuba pamoja na andiko moja au mawili ya msingi. Kwa hiyo, tutakuwa na habari nzuri sana za kuzungumzia wakati wa jioni ya Ibada ya Familia majuma kadhaa kabla ya kuhudhuria kusanyiko. Wahubiri wengine huchapisha programu hiyo na kuitumia wanapoandika mambo makuu wakati wa kusanyiko.

4. Kusanyiko linawezaje kuwasaidia wazazi wawafundishe watoto wao?

4 ‘Wafundisheni Wana Wenu’: Kusudi moja la kusanyiko lililofanywa kwenye Mlima Sinai lilikuwa kuwatia moyo wazazi Waisraeli “wawafundishe wana wao.” (Kum. 4:10) Kusanyiko huwapa wazazi fursa ya pekee ya kufanya vivyo hivyo. Wazazi wanapaswa kuketi pamoja na watoto wao wakati programu inaendelea na kuwasaidia wawe makini. Familia zinaweza kuzungumzia programu mwishoni mwa kila siku ya kusanyiko na baadaye wakati wa ibada ya familia.

5. Tutanufaikaje kwa kuhudhuria kusanyiko lijalo?

5 Kusanyiko la kihistoria kwenye Mlima Sinai liliwasaidia Waisraeli wathamini pendeleo lao la pekee la kuwa watumishi wa Mungu. (Kum. 4:7, 8) Kusanyiko lijalo limekusudiwa kutunufaisha kwa njia hiyohiyo. Katika siku hizo tatu, kwa njia ya mfano tutaweza kutoka kwenye ulimwengu mkatili wa Shetani na kufurahia burudisho la kiroho na ushirika wenye kujenga katika paradiso ya kiroho. (Isa. 35:7-9) Kadiri siku ya Yehova inavyokaribia, tusipuuze kamwe fursa hiyo ya kukusanyika pamoja kwa ajili ya badilishano la kitia moyo!—Ebr. 10:24, 25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki