Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/02 uku. 1
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari Zinazolingana
  • Mkusanyiko Ambao Uliongeza Itibari Yetu Katika Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Unaweza Kuwatumaini Ndugu Zako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Kuwatumaini Wengine Ni Muhimu kwa Maisha Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 7/02 uku. 1

Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko

1 Ili tusimame imara katika imani katika ulimwengu huu wenye msukosuko, lazima tumtumaini Yehova. Hiyo yamaanisha nini maishani? Kumtumaini Yehova kuna matokeo gani kwetu binafsi na kwa familia yetu? Hutusaidiaje kukinza uvutano wa ulimwengu wa Shetani? Programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2003 yajibu maswali hayo. Kichwa chake ni “Mtumaini Yehova Ukatende Mema.”—Zab. 37:3.

2 Hatumtumaini Yehova wakati wa pindi za pekee tu au nyakati za uhitaji wa dharura. Sisi humtumaini katika maisha yetu kila siku. Hilo lakaziwa katika hotuba ya kwanza, “Mtumaini Yehova Nyakati Zote.” (Zab. 62:8) Mfululizo wa hotuba nne wenye kichwa “Kuonyesha Tunamtumaini Yehova” utatuonyesha jinsi ya kupata na kutumia habari inayotegemea Biblia inayoweza kutusaidia tuimarishe ndoa yenye mafanikio, kushughulikia matatizo yanayotokea katika familia, na kutimiza mahitaji yetu ya kimwili.

3 Ulimwengu wa Shetani unajaribu kutulemea na maoni yaliyopotoka kuhusu lililo sawa na lililo baya na kutuvuruga tusione ni mambo gani yaliyo ya maana. (Isa. 5:20) Hotuba yenye kichwa “Jihadharini na Mambo ya Ubatili” na “Epukeni Mabaya—Tendeni Mema” zitakaza kikiki azimio letu la kushikilia viwango vya juu vya Yehova.—Amo. 5:14.

4 Yehova atakapoharibu ulimwengu wa sasa ulio mwovu, watumishi wake watahitaji kumtumaini kabisa. Hilo lakaziwa kwenye hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Ukombozi Kutoka Katika Taabu za Ulimwengu U Karibu.” Baada ya hapo, tutaombwa kujichunguza wenyewe katika sehemu yenye kichwa “Je, Utahesabiwa Kuwa Unastahili Ufalme wa Mungu?” Programu itamalizia kwa sihi hii “Tumaini Ahadi za Yehova.”

5 Jambo kuu la kila kusanyiko huwa ni hotuba ya ubatizo. Yeyote anayetaka kubatizwa anapaswa kumwambia mwangalizi-msimamizi upesi iwezekanavyo ili mipango inayohitajiwa ifanywe.

6 Katika nyakati hizi zisizo na uhakika, Yehova ndiye chanzo pekee cha uhakika na uthabiti. (Zab. 118:8, 9) Sisi sote na tuimarishe tumaini letu kwake kwa kuhudhuria programu yote ya kusanyiko la mzunguko.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki