Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee
1 Ingawa vyombo vya habari na walimu wa kilimwengu hutukuza utajiri wa vitu vya kimwili, Neno la Mungu hutusihi ‘Tuwe Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora.’ (1 Tim. 6:18) Hicho ndicho kichwa cha programu ya kusanyiko la pekee inayoanza Septemba 2002. Tutapata kitia-moyo gani kusanyikoni?
2 Mwangalizi wa mzunguko atazungumzia maana ya ‘Kuwa Matajiri Machoni pa Mungu,’ naye atawahoji watu fulani ambao wanajitahidi sana kupata utajiri wa kiroho. Msemaji anayezuru ataonyesha katika hotuba yake ya kwanza siku hiyo, jinsi watu wa Mungu wanavyofanya “Kazi Zilizo Bora Wakati Huu wa Mavuno.” Kila mmoja wetu atatiwa moyo kuchunguza jinsi anavyoweza kushiriki hata zaidi katika kazi ya mavuno ambayo Mungu ametupa leo.
3 Sisi huona fahari sana vijana wanapofuatia utajiri wa kiroho! Hilo humtukuza Yehova na husaidia vijana waweke msingi bora wa mapendeleo ya utumishi ya wakati ujao. Sehemu yenye kichwa “Kuwapongeza Vijana kwa Kazi Zilizo Bora za Kumsifu Yehova” itakazia kazi zilizo bora ambazo vijana Wakristo wa kwenu wamekuwa wakifanya.
4 Matokeo ya kufuatia kazi zilizo bora ni yapi? Msemaji anayezuru atazungumzia hilo katika hotuba yake ya mwisho, “Endeleeni Kufanya Kazi Zilizo Bora na Kupata Baraka za Yehova.” Atazungumzia sehemu nne ambazo twapokea baraka tele: (1) tukiwa mtu mmoja-mmoja, (2) tukiwa familia, (3) tukiwa kutaniko, na (4) tukiwa tengenezo la ulimwenguni pote.
5 Wale ambao wamejiweka wakfu kwa Yehova watakuwa na fursa ya kubatizwa. Ikiwa uko tayari kuchukua hatua hiyo, mjulishe mwangalizi-msimamizi mara moja.
6 Tarehe ya kusanyiko lenu ikitangazwa, fanya mipango hususa haraka ili uhudhurie. Jitahidi kufika mapema ili ushiriki wimbo na sala ya kufungua. Kuhudhuria na kusikiliza kwa makini programu yote ya kusanyiko la pekee kutatuimarisha twendelee kufuata mwendo utakaotufanya tuwe matajiri kikweli machoni pa Mungu wetu, Yehova.