Madokezo ya Kutoa Kitabu Mkaribie Yehova
◼ Ukiwa na Biblia mkononi, sema: “Watu wengi ambao humwamini Mungu wangependa kumkaribia. Je, ulijua kwamba Mungu anatualika tumkaribie? [Soma Yakobo 4:8.] Kichapo hiki kimekusudiwa kuwasaidia watu watumie Biblia yao wenyewe kumkaribia Mungu.” Soma fungu la 1 kwenye ukurasa wa 16.
◼ Ukiwa na Biblia mkononi, sema: “Leo ukosefu wa haki umezidi. Ni kama tu inavyofafanuliwa hapa. [Soma Mhubiri 8:9b.] Watu wengi wanajiuliza kama kweli Mungu anajali. [Soma sentensi mbili za kwanza za fungu la 4 kwenye ukurasa wa 119.] Sura hii yaelezea ni kwa nini Mungu ameruhusu ukosefu wa haki kwa muda fulani.”