Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/04 uku. 6
  • Faidika kwa Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Faidika kwa Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • “Kilijaza Pengo Fulani Moyoni Mwangu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Tutaanza Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova Juma Linaloanza Januari 6
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Kujifunza Kitabu Mwabudu Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 2/04 uku. 6

Faidika kwa Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova

1 Katika Kusanyiko la Wilaya la “Watangazaji wa Ufalme Wenye Bidii,” tulifurahi kupokea kitabu Mkaribie Yehova. Wengi walikisoma kitabu hicho mara moja. Bila shaka andiko la mwaka la 2003 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia” liliwachochea wengine wengi kukisoma.—Yak. 4:8.

2 Katika mwezi wa Machi, tutaanza kujifunza kitabu Mkaribie Yehova katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Tunaweza kufaidikaje kikamili na funzo letu? Ni muhimu kutayarisha. Majuma mawili yatatumiwa kujifunza kila sura, kukiwa na mafungu machache yaliyoratibiwa kusomwa kila juma. Hiyo itakupa wakati wa kutosha kutoa maelezo yanayotegemea funzo lako na kutafakari kwako habari hiyo. Zaidi ya hayo, mafungu machache hata zaidi yatachunguzwa katika majuma ambayo umalizio wa sura unapitiwa, ili kuruhusu wakati wa kutumia sehemu ya pekee ya kitabu hicho.

3 Kuanzia sura ya 2, sanduku linaloitwa “Maswali ya Kutafakari” linapatikana karibu mwishoni mwa kila sura. Baada ya kuchunguza fungu la mwisho katika sura, mwangalizi wa funzo la kitabu ataruhusu kikundi kizungumzie sanduku hilo. Atawatia moyo washiriki wa funzo la kitabu watoe maoni, akitafuta matokeo mazuri ya kutafakari kwao juu ya Maandiko. (Met. 20:5) Mbali na maswali yaliyo katika sanduku, nyakati nyingine anaweza kuuliza maswali kama vile: ‘Habari hii inakufundisha nini juu ya Yehova? Ina matokeo gani katika maisha yako? Unaweza kuitumiaje ili kuwasaidia wengine?’ Mradi wake utakuwa kupata maelezo yao ya kutoka moyoni, wala si kufanya mtihani kuhusu mambo madogo-madogo.

4 Mkaribie Yehova ni kitabu cha pekee. Ingawa vichapo vyote vya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” humtukuza Yehova, kitabu hiki kimeandaliwa hasa kuzungumzia sifa za Yehova. (Mt. 24:45-47) Tuna pendeleo zuri kama nini mbele yetu! Tutafaidika sana kwa kujifunza kindani utu wa Yehova. Funzo hilo na litusaidie kumkaribia zaidi Baba yetu wa mbinguni, na tuwe na matokeo zaidi tunapowasaidia wengine kufanya hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki