Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Apr. 15
“Miaka ya karibuni watu wengi wameona kwamba maadili ya kiroho yamepotoka. Je, umeona jambo hilo? [Ngoja ajibu. Kisha soma Zaburi 119:105.] Maadili ya kiroho yanaweza kusaidia watu waepuke mitego maishani. Gazeti hili laonyesha mahali tunakoweza kupata maadili ya kiroho.”
Amkeni! Apr. 22
“Katika ulimwengu wa leo wenye hekaheka nyingi, wengi wanajiuliza kama watoto wanakua haraka mno au vipi. Je, unahangaishwa na jambo hilo? [Ngoja ajibu. Kisha soma Mhubiri 3:1, 4.] Wakati wa utotoni haupaswi kuwa wakati wa kubeba madaraka mazito ya watu wazima. Toleo hili la Amkeni! lazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kulinda hali ya utotoni ya watoto wao.”
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Maswali mengine hayawezi kujibiwa na mwanadamu. Ona mfano mmoja. [Soma Ayubu 21:7.] Je, umewahi kuwa na swali ambalo ungependa kumwuliza Mungu? [Ngoja ajibu.] Gazeti hili laeleza jinsi ambavyo watu kutoka sehemu zote duniani wamepata majibu yenye kuridhisha kwa maswali matatu muhimu maishani.”
Amkeni! Mei 8
“Wengi wetu twamjua mtu fulani aliye na ugonjwa wa kisukari. Je, unajua mengi kuhusu ugonjwa huo? [Onyesha jalada la gazeti, na ungoje jibu.] Gazeti hili limechunguza visababishi na tiba ya ugonjwa wa kisukari. Pia lazungumzia ahadi ya Biblia ya tiba ya kudumu ya magonjwa yote.” Malizia kwa kusoma Isaya 33:24.